ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, September 5, 2018

OSHA KUZIPIGA FAINI TAASISI ZITAKAZOSHINDWA KUJISAJILI MPAKA DISEMBA 2018



 GSENGOtV
Wakala wa usalama mahala pa kazi nchini OSHA unatarajia kuanzisha oparesheni maalum kwa waajiri wote ili kuhakikisha ikiwa wamejisajili na wakala huo kama ilivyo matakwa ya kisheria.
Kaimu Mtendaji Mkuu OSHA, Khadija Mwenda ameyasema hayo hii leo kwenye semina/ kikao kazi na wanahabari mkoani Mwanza, kilichofanyika katika ukumbi wa Nyakahoja.
Amesema katika kuboresha mazingira ya ufanyaji kazi nchini, OSHA imeondoa gharama za ujali kwa kila mwajiri lakini bado mwitikio kwa waajiri kujisajili bado ni mdogo hivyo wakala huo umepanga kuanza oparesheni maalum kuanzia mwezi huu hadi Disemba ili kuhakikisha kila mwajiri anasajiliwa.
Mwenda amesema ikiwa mwajiri atakutwa hajajisajili OSHA hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake hivyo waajiri wote wahakikishe wanasajiliwa kabla oparesheni hiyo haijawafikia kwani kujisajili ni bure.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.