ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, September 2, 2018

BREAKING NEWS: WATU WAWILI WAFARIKI KATIKA AJALI YA GARI LILILOSHIKA MOTO.


Picha ya mtandao

Watu wawili wamefariki na wengine wawili kujeruhiwa usiku wa kuamkia leo huko Dunga, Zanzibar, baada ya gari walilokuwa wakisafiria kushika moto.

Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema gari hilo aina ya Toyota IST lililokuwa likitokea Kiwengwa, lililipuka baada ya tenki lake la mafuta kuvuja kufuatia kugongwa na jiwe.

Majina ya waliofariki na kujeruhiwa yalikuwa hayajapatikana hadi tunakwenda mitamboni.  Hata hivyo, tutawajuza wasomaji wetu mara tu tukipata habari zaidi kuhusu tukio hilo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.