ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 29, 2018

MASHABIKI WA MANCHESTER UNITED WANATAKA KUONA NINI MOURINHO ANAWAFANYIA ZAIDI YA KUJUA HISTORIA YAKE.



GSENGOtV
Taarifa za andani ya klabu ya Manchester United zinaeleza kuwa wachezaji wa timu hiyo pamoja na wafanyakazi wanaamini meneja wao Jose Mourinho huwenda akatimuliwa kazi endapo atapoteza katika mchezo wao wa Jumapili ya terehe 01/09/ 2018 dhidi ya Burnley.

Kiongozi wa United, Ed Woodward amefanya mazungumzo na Mourinho juma hili kufuatia timu yao kupata matokeo mabaya mfululizo dhidi ya Brighton na Tottenham.

Wachambuzi wa mambo wanaamini kikao hicho kinafanana na kile alichofanyiwa meneja, Louis van Gaal katika siku zake za mwisho mwaka 2016 na nafasi yake kuchukuliwa na Mourinho ambaye kwa sasa kunauwezekano mkubwa wa Zinedine Zidane kurithi mikoba hiyo.

Chanzo hicho kutoka ndani ya Manchester United kimesema kuwa ”Muda si mrefu, Jose atatimuliwa wengine wakiamini ataondoka endapo atapoteza mbele ya Burnley na wengine wakiamini hatokuwepo mwanzoni mwa mwezi wa tisa ,” kimesema chanzo hicho.

Inaelezwa kuwa wachezaji nane pekee ndiyo waliyoungana meneja wao, Mourinho kutoka kwenye viunga vya Carrington kwenda kwenye hoteli yao ya the Lowry baada ya kumalizika kwa mechi yao na Spurs wakati wengine wakiamua kuondoka binafsi huku Paul Pogba akitumia gari lake.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.