ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 29, 2018

MADUKA 10 YATIWA KUFULI, UKAGUZI WA WAUZAO DAWA ZA MIFUGO MKOANI MWANZA



NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV
Baraza la vetenari nchini limeyafunga maduka kumi ya pembejeo za mifugo jijini mwanza baada ya kubaini kuwa maduka hayo hayana leseni ya kufanya biashara ya kuuza pembejeo pamoja na kutokuwa na wataalam wa mifugo.

Mkaguzi wa baraza hilo DKT.GEORGE MTINDA amesema kuwa wamiliki wa maduka yaliyofungiwa watalazimika kulipa faini pamoja na kuajiri wataalam wa mifugo ili yaweze kuendelea na biashara ya pembejeo.

Katika msako huo, Baraza hilo limebaini maduka 10 ambayo hayana wataalam wa mifugo na leseni za kuendesha biashara ya dawa za mifugo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.