ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 14, 2018

SERIKALI YADHAMIRIA KUPUNGUZA VIFO VYA MAMA MJAMZITO NA MTOTO MCHANGA MWANZA

Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazaee na watoto Ummy Mwalimu amesema licha ya kuwepo kwa changamoto nyingi za upatikanaji wa huduma za afya nchini serikali imejipanga kupunguza magonjwa na vifo vya mama mjamzito na mtoto mchanga kwani sababu zinazochangia vifo hivyo zinaweza kuzuilika.

Akizindua mradi wa impact unaolenga kupunguza magonjwa na vifo vitokanavyo na uzazi kwa mama mjamzito na mtoto mchanga Waziri wa Afya, Jinsia wazee na watoto ummy mwalimu amesema sekta ya afya bado inakabiliwa na changamoto huku akiahidi kuendelea kushirikiana na wadau kuzitatua. BOFYA KUMSIKILIZA Ummy Mwalimu……Waziri wa Afya,Jinsia,Wazee na watoto



Akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mary Tesha ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana na Mbunge wa Jimbo hilo Stanslaus Mabula wanaelezea taarifa ya utoaji wa huduma za Afya Mkoani Mwanza



Vifo vitokanavyo na uzazi bado ni tatizo,huku takwimu za kitaifa zikionyesha akina mama 556 hupoteza maisha katika kila vizazi  hai laki moja na kwa Mkoa wa Mwanza vifo vimeongezeka kutoka 150 hadi vifo 195 katika vizazi hai laki moja,Ambavyo husababishwa kupoteza damu nyingi kabla na baada ya kujifungua,kifafa cha mimba,uchungu pingamizi na vifo vya watoto njiti na wanaoshindwa kupumua.

Hapa Ummy Mwalimu anatoa onyo kwa waganga wakuu na kuelezea mikakati ya serikali katika kuboresha huduma ya mama na mtoto

Mradi huo wa miaka minne wa Afya ya uzazi mama mjamzito na mtoto mchanga unaofadhiliwa na serikali ya Canada pamoja na shirika la Aghakan utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 25.3 za kitanzania na unalenga kuwafikia wanawake wenye umri wa kuzaa 650,000.




















Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.