ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, July 5, 2018

'NZIGE WATU' WAZIPA PRESHA KAYA ZA WAKULIMA WILAYANI MISUNGWI.



NA ZEPHANIA MANDIA GSENGOtV
Baada ya wanawake wanaouza miili yao maarufu kwa jina la "NZIGE" kuvamia wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, Serikali imewataka wanaume wilayani humo, kuachana na tabia mbovu ya kutumia fedha za mauzo ya mazao yao kwa matumizi ya anasa.

Kutokana na uvamizi huo katika kata ya NUNDULU, kupitia Uzinduzi wa kampeni ya miezi miwili, Serikali imewataka wanaume kutumia fedha kuendeleza familia kwa kujenga nyumba bora na kusomesha watoto, waliotelekezwa bila malezi bora ya wazazi.

Juma Sweda ni Mkuu wa wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, ameshiriki mstari wa mbele kuzindua kampeni maalum ya kutokomeza aina zote za ukatili wa kijinsia wilayani humo itakayodumu kwa kipindi cha miezi miwili.










Wilaya ya MISUNGWI ni miongoni mwa maeneo ya mkoa wa MWANZA, ambayo wakazi wake licha ya kuzalisha kwa wingi mazao ya chakula na biashara, lakini wameendelea kuishi katika duni.
Maisha hayo yanatokana na baadhi ya wanaume kutumia fedha za mauzo ya mazao kwa matumizi ya anasa, na kusababisha wazazi wengi kushindwa kusomesha watoto na kulalia magodoro yaliyotengenezwa kwa nyasi maarufu kama DODOMA NGUBALU.
Kwenye uzinduzi huo, baadhi ya wanaume wamekiri kutumia fedha zinazotokana na mauzo ya mazao kwa mambo ya anasa halmashauri

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.