ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, July 11, 2018

VIDEO:- GARI LA KUBEBEA WAGONJWA LA HOSPITALI YA WILAYA YA TARIME LIMENASWA LIKISAFIRISHA KILO 800 ZA DAWA ZA KULEVYA AINA YA MIRUNGI



NA ZEPHANIA MANDIA GSENGOtV

Baada ya serikali kuimarisha mapambano dhidi ya biashara haramu ya dawa za kulevya,baadhi ya watu wanaamini zama ni zile zile kwa tafsiri tu ilimradi mkono uende kinywani.ni tukio la aina yake, likiibua mitazamo hasi kwa kila aliyelishuhudia ama kulisikia.

Gari la hospitali ya wilaya tarime iliyozoeleka kubeba wagonjwa mahututi leo imenaswa wilayani bunda ikisafirisha shehena ya dawa za kulevya aina ya mirungi kutoka wilayani tarime kwenda jijini mwanza kutafuta soko.

Shehena hiyo imekamatwa wilayani bunda mkoani mara ikiwa ndani ya gari hilo lililokuwa limewasha alama za kuonyesha kuwa na mgonjwa.

Akizungumza baada ya kushuhudia shehena hiyo,Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama,mkuu wa  mkoa wa Mara ADAM MALIMA amewaonya wale wote wanaojihusisha na biashara ya madawa ya kulevya.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa mara JUMA NDAKI jeshi hilo linawashikilia watu wawili akiwemo dereva wa gari hilo la wagonjwa GEORGE MATAI ambaye licha ya kutakiwa kuchukua mgonjwa mahututi toka hosptali ya Tarime na kumpeleka Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza alitoa visingizio juu ya gari kutokuwepo na baadae kubainika akiwa na dawa za kuleva wilayani Bunda huku akiwa amewasha alamu kuonyesha yupo na mgonjwa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.