ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 30, 2018

RC MAKONDA APOKEA SHEHENA YA VIFAA VYA MATIBABU KUTOKA KOREA KUSINI.

 NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mhe. Paul Makonda* leo amepokea *shehena ya Vifaa vya matibabu* vyenye thamani ya shilingi *milioni 100* kutoka serikali ya *Korea Kusini* kupitia shirika la *KOICA*.

Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na *Digital X-ray 3, Ultrasound 1, Kabati la usalama wa viumbe* (safety cabinet) 1, *Mashine 3 za kupima mkojo, mashine ya kuwapa joto watoto njiti* (baby warmer) pamoja na *mashine ya utakitshaji.*
 Baada ya kupokea vifaa hivyo kutoka kwa *Balozi wa Korea kusini Bwana Geum Young Song RC Makonda* amekabidhi vifaa hivyo kwenye *vituo vya Afya vya Sinza, Mnazi Mmoja na Mbagala* ambako kuna uhaba wa vifaa. 

 Kabla ya kupokea vifaa hivyo *RC Makonda* alifanya *mazungumzo* na *Balozi* huyo wa Korea kusini na kuwasilisha *ombi la kujengwa kwa Chuo cha kisasa cha mafunzo ya udaktari na uuguzi* ambapo *Balozi Geum Young Song amepokea kwa mikono miwili ombi hilo.*
 *RC Makonda* pia amemueleza Balozi ombi la kujengwa kwa *kituo kikubwa cha upimaji wa magonjwa mbalimbali* kwa wananchi kwenye *eneo moja* ambapo pia Balozi *amepokea* ombi hilo na kumsifu *RC Makonda* kwa moyo wake wa kujali wananchi. 



Kwa upande wake *Balozi* wa Korea Kusini nchini Tanzania *Bwana Geum Young Song* amesema wametoa vifaa hivyo *kuunga mkono kazi kubwa inayofanywa na Mkoa wa Dar es salaam katika uboreshaji wa sekta ya Afya* na wataendelea kusaidiana na serikali.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.