ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 30, 2018

"SERA YA SERIKALI YA VIWANDA ISITUMIKE KAMA MWANYA WA UANZISHWAJI VIWANDA BUBU' - WASEMA WADAU



NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV
Kakika juhudi za kumuunga mkono RAIS MAGUFULI kuelekea tanzania ya viwanda, Serikali imeombwa kuwajengea uwezo wajasiriamali na kuondoa bidhaa feki kwenye soko pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria wafanyabiashara wanaonakili nembo na uzalishaji wa bidhaa zao  kinyume cha sheria.

Kilio hicho kimetolewa na wafanyabishara wa jijini Mwanza wanaozalisha vinywaji aina ya Wine zinazotokana na matunda pamoja na mtama.

Aidha meneja wa (TFDA) kanda ya ziwa MOSES MBAMBE,amewataka wananchi  kutoa ushirikiano pale wanapoona bidhaa ambayo wanaitilia sahaka nakuwataka wajasilia mali kurasimisha bidhaazao ili zitambulike na (TFDA) pia mbambe amesema kwa sasa wanaendelea kutoa elimu kwa wajasiliamali wa kanda ya ziwa.

Mkurugenzi wa kiwanda cha Mwanza quality wine Leonald Lema amesema kuwa   mamlaka zinazohusika zinapashwa kuingilia kati kwani bidhaa feki zinawaathiri wao pia maptao kodi ya serikali.

Aidha LEMA amebainisha kuwa kiwanda chake hakina tatizo la vifungashio tatizo ambalo limekuwa likipigiwa kelele kuwa bidhaa nyingi hapa nchini zinakosa ubora katika ushindani kwenye soko ukilinganisha na bidhaa toka nje.

Naye Mkurugenzi wa FARU WINES Japhet Daniel amesema kuwa serikali kwa kutumia mihili yake inaweza kuwatambua wajasiriamali wasio sajiliwa kutumia vifungashio vya bidhaa za FARU BANANA.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.