ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 10, 2018

TRUMP: KUNA UWEZEKANO NIKAVUNJA AJENDA YA KUKUTANA NA KIONGOZI WA KOREA KASKAZINI.

Trump: Kuna uwezekano nikavunja ajenda ya kukutana na kiongozi wa Korea Kaskazini




CHANZO/PARStODAY
Rais Donald Trump wa Marekani sambamba na kusema kuwa, ataweka wazi siku tatu zijazo nukta atakazozijadili pamoja na Kiongozi wa Korea Kaskazini, amesema kuwa, ni suala linalowezekana kuvunja ajenda ya mkutano huo.
Trump ameyasema hayo huku Mike Pompeo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani akiwa amefanya safari mjini Pyongyang na kukutana na Kim Jong-un. Akizungumza na waandishi wa habari waliomuuliza iwapo anaweza kuvunja kikao tarajiwa na kiongozi huyo wa Korea Kaskazini, Trump hakukadhibisha suala hilo. Amesema kuwa, pande zote mbili yaani (Washington na Pyongyang) zinataka kufikia makubaliano.
Kim Jong-un, Kiongozi wa Korea Kaskazini
Serikali ya Korea Kaskazini imeionya Marekani kwamba sambamba na kukaribia kikao cha viongozi wakuu wa nchi hizo, Washington inatakiwa ijiepushe na uharibifu wowote wa anga ya mazungumzo hayo tarajiwa. Taarifa iliyotolewa na chama tawala nchini Korea Kaskazini imeashiria matamshi ya kila mara ya kupenda kujitanua yanayotolewa na viongozi wa Marekani hususan yanayosisitizia kuwekewa zaidi mashinikizo serikali ya Pyongyang. Kuhusiana na suala hilo chama hicho tawala nchini Korea Kaskazini kimesema kuwa ni muhimu sana kwa Marekani kujiepusha na anga ambayo inaweza kudhoofisha kufanyika mazungumzo tarajiwa kati ya Rais Donald Trump na Kim Jong-un.
Trump ni mtu asiyeaminika hata kidogo
Taarifa hiyo imeendelea kufafanua kuwa, iwapo miamala hiyo ya uhasama itaendelea dhidi ya Pyongyang, basi ni Marekani yenyewe ndiyo itakayopata hasara. Weledi wa mambo wanaamini kwamba, hatua ya siku ya Jumanne ya Trump katika kuiondoa nchi yake katika makubaliano ya nyuklia ya Iran JCPOA, imewafanya viongozi wa Korea Kaskazini kutokuwa na imani hata kidogo na Marekani kutokana na miamala yake ya kukiuka makubaliano. Trump na Kim Jong-un wanatazamiwa kukutana mwishoni mwa mwezi huu, au mwanzoni mwa mwezi Juni.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.