ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 4, 2018

VIDEO: BABU SEYA NA BENDI YAKE WAKARIBISHWA DINNER NA DIAMOND LOUNGE MWANZA


Baada ya ya kutinga jijini Mwanza marafiki wa kiota cha burudani kilicho maarufu jijini hapa kinachopatikana kona ya Bwiru wilayani Ilemela, Diamond Lounge wamesema katu lazima wa-show love na Babu Seya na Mwanae.

Hapa ni sehemu ya hafla kimya kimya ya chakula cha jioni ambapo uongozi wa eneo hilo umehaidi mara baada ya kumaliza show zao kwa mikoa ya Geita (leo ijumaa) na Mwanza (kesho jumamosi) watawazawadia ndoo za samaki wanamuziki hao wakati wakirejea jijini Dar es salaam.
Ujio wa mwanamuziki Nguli wa muziki wa Dansi nchini Tanzania Nguza Viking al maarufu Babu Seya akiwa na mwanaye Papii Kocha unakuja  ikiwa ni kwaajili ya kuikata ile kiu ya muda mrefu ya burudani ya muziki wa ukweli waliyoikosa kwa takribani miaka 14 wakati wakali hao walipokuwa wametupwa gerezani.

HISTORIA
Mnamo Tarehe 9 Mwezi Disemba 2016 msamaha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli uliwajumuisha mwanamziki maarufu nchini Tanzania Nguza Viking, maarufu kama Babu Seya aliyehukumiwa kifungo cha maisha jela.
Msamaha huu unatajwa kuwa historia na hasa kuwasamehe wafungwa wa maisha na wale wa kunyongwa ambapo kwa wakunyongwa waliachiwa huru ni 61 na wengine walioachiwa huru kutokana na makosa mbali mbali ni 1,821 huku wengine 8157 wamepunguziwa adhabu zao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.