ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 15, 2018

VIDEO:- BARCA ILIVYOIADHABISHA VIBAYA CHELSEA



Meneja wa Chelsea Antonio Conte amesema alihisi kwamba kichapo cha 3-0 ambacho klabu yake ilipokezwa katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Jumatano "hakikuwa cha haki".
Lionel Messi alifunga mabao mawili naye Ousmane Dembele akafunga moja - bao lake la kwanza akichezea Barca - na kuwasaidia miamba hao wa Uhispania kuondoka na ushindi wa jumla wa 4-1.
Mechi ya kwanza uwanjani Stamford Bridge ilikuwa imemalizika 1-1.
Matokeo hayo yaliwaondoa Chelsea kutoka kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya msimu huu na msimu ujao wanakabiliwa na kibarua cha kufuzu kutokana na ushindani mkali kwenye nafasi nne za kwanza Ligi ya Premia.
"Hatuna majuto," alisema Conte.
"Ukiitazama mechi hiyo, utaona kwamba matokeo hayo hayakuwa ya haki."

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.