ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 16, 2018

VICHWA VYABAKI NA MASWALI KIFO CHA MFANYABIASHARA WA MABASI JIJINI MWANZA


HATIMAYE mwili wa aliyekuwa mfanyabiashara maarufu wa mabasi jijini Mwanza Samson Josiah ambaye alikuwa mmiliki wa Kampuni ya mabasi ya abiria ya Super Sami, umezikwa leo katika makaburi ya kikristo yaliyoko wilayani Magu mkoani Mwanza.

Majira ya saa 9:30 alasili mwili wa mfanyabiashara huyo ulishushwa na kuhifadhiwa kwenye nyumba yake ya milele ikiwa ni mara baada ya ibada ya mazishi iliyotangulia ikiongozwa na Mchungaji Jackson Meza kutoka Kanisa la African Inland Church of Tanzania (AICT) kufanyika nyumbani kwake alikokuwa akiishi mtaa wa Majengo Mapya wilayani Magu.

Kwaya ya kanisa ambayo marehemu alikuwa mfadhili wake iliimba nyimbo za maombolezo zenye hisia na hata kusababisha maelfu ya wa waombolezaji wamemiminika kutoka sehemu mbalimbali kuangua kilio kwenye ibada hiyo.

Hata hivyo mwili wa marehemu Josiah haukuweza kufunguliwa katika jeneza lake na kuagwa kwa njia za kawaida kama zilivyo taratibu za imani ya kikristu kutokana na taarifa kutoka kwa ndugu wa marehemu kusema kuwa mwili wa ndugu yao ulikuwa umeharibika sana. 

Jembe Fm kupitia mwanahabari wake Albert G. Sengo imefanya mazungumzo na Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara Jafar Mohamed:- (FUATILIA SAUTI YA VIDEO HAPO JUU)


Mwili wa mfanyabiashara huyo uliokutwa ukiwa umefungwa kwenye viroba ukielea ndani ya Mto Ndabaka mpakani mwa wilaya za Bunda mkoa wa Mara na Busega mkoani Simiyu umewasili asubuhi ya leo Machi 16 ukitokea Hospitali ya Rufaa Mara ulikohifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi tangu juzi.

Marehemu Josia aliyezaliwa mwaka 1968 alipotea tangu Februari 27 kabla ya gari lake kukutwa likiwa limeteketezwa kwa moto ndani ya eneo  la hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara Machi 9.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.