ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 13, 2018

UVUVI HARAMU BADO TISHIO MKOANI MWANZA WANNE WABAMBWA.



Watu wanne wamenaswa pembezoni mwa Ziwa Victoria wakijihusisha na uvuvi uliopigwa marufuku na Serikali.

Uvuvi katika Ziwa Victoria ni shughuli kubwa ya kiuchumi na chanzo muhimu cha mapato kwa jamii husika na kampuni za kibiashara. Hali halisi ni kwamba jamii inayoishi kando ya Ziwa Victoria, inategemea uvuvi kama shughuli kuu za kiuchumi.

Licha ya umuhimu huo, kiwango cha samaki kinachotakiwa kubaki ziwani kimepungua kupita kiasi kwa miongo kadhaa. Tathmini ya kiasi cha samaki kinachotakiwa kubaki ziwani, iliyofanywa na Taasisi ya Uvuvi Ziwa Victoria (LVFO), inaonesha mwenendo wa kupungua kwa samaki sangara tangu mwaka 2000.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.