ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 1, 2017

MAFURIKO NIGERIA YAPELEKEA WATU 110,000 KUPOTEZA MAKAZI.

Mafuriko Nigeria yapelekea watu 110,000 kupoteza makazi
Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria amesema watu zaidi ya laki moja na elfu kumi wamepoteza makazi yao baada ya kutokea mafuruko katika jimbo la Benue katikati mwa nchi hiyo.
Katika taarifa ya siku ya Ijumaa kupitia akaunti yake ya Twitter, Rais Buhari amesema timu za uokoaji zimefika katika eneo la maafa kusaidia familia za waathirika.
Hadi hivi sasa hakuna taarifa kamili kuhusu hasara iliyopatikana kufuatia mafuriko hayo.
Tokea mwanzoni mwa mwaka huu, Nigeria imekumbwa na mvua kali za msimu ambazo zimesababisha hasara katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi.
Rais Buhari wa Nigeria.
Jimbo la Benue linategemea sana kilimo na hukumbwa na mafuriko mara kwa mara kutokana na mvua kali na kufunguliwa mabwawa ya nchi jirani ya Cameroon. Mwaka 2012 Nigeria ilikumbwa na mafuruko mabaya katika majimbo 30 kati ya 36 ya nchi hiyo. Mamia ya watu waliaga dunia na wengine milioni mbili kuachwa bila makazi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.