ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 10, 2017

UPINZANI AFRIKA KUSINI WATAKA BUNGE LIVUNJWE.


Chama cha upinzani nchini Afrika Kusini cha Democratic Alliance (DA) kimetoa wito wa kuvunjwa Bunge la nchi hiyo na kufanyika uchaguzi mpya.
Wito huo umetolewa siku moja baada ya kushindwa kwa hoja ya kambi ya upinzani ya kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais Jacob Zuma wa nchi hiyo. 
Mkuu wa chama cha upinzani cha DA, Mmusi Maimane amesema kuwa chama hicho leo kitawasilisha bungeni hoja ya kulivunja Bunge na ameomba hoja hiyo ijadiliwe haraka iwezekanavyo.
Rais Jacob Zuma wqa Afrika Kusini ambaye anakabiliwa na tuhuma za ufisadi na kutumia vibaya madaraka amenusurika kura ya kutokuwa na imani naye na kuondolewa madarakani. Hata hivyo kiongozi huyo amejeruhika kisiasa baada ya baadhi ya wanachama wa chama chake tawala cha ANC kuungana na upinzani na kupiga kura dhidi yake.
Rais Zuma wa Afrika kusini ambaye amenusurika kura ya kuondolewa madarakani.
Maimane amewaambia waandishi wa habari katika mji wa Cape Town kwamba matokeo ya kura za wabunge yameonyesha kuwa, chama cha ANC kimegawanyika na nchi inahitaji mwanzo mpya.
 
Mkuu huyo wa chama cha upinzani cha Democratic Alliance amesema anaamini kuwa, Bunge linapasa kuvunjwa ili nchi hiyo iitishe uchaguzi wa mapema.
Kipindi cha utawala wa Zuma kitamalizika mwaka 2019.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.