ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 23, 2016

SHIRIKA LA NDEGE LA ETIHAD LAINGIA MAKUBALIANO YA KIHISTORIA NA 'Precision Air'

KATIKA hatua za kuhakikisha inayafikia maeneo mengi Afrika Mashariki, Shirika la Etihad la Umoja wa Falme za nchi za Kiarabu limeingia makubaliano na Shirika la ndege la hapa nchini Precision Air ambayo yamelenga kupanua huduma zaidi ndani na nje ya Tanzania.

Makubaliano hayo yanatoa fursa kwa, Shirika la Ndege la ‘Precision Air’ ambalo linaongoza kwa utoaji huduma hapa nchini kuweza kutoa huduma za moja kwa moja katika nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu na zaidi.

Kupitia makubaliano hayo, Shirika la Ndege la Etihad litaweka alama yake ya kibali EY kwenye ndege za ‘Precision Air’ zinatoa huduma kati ya Dar es Salaam, Kilimanjaro, Mwanza, Mtwara, Nairobi, Zanzibar na Pemba, Vilevile kwenye ndege zinazotoa huduma kati ya Nairobi, Kilimanjaro na Zanzibar.

Aidha, Precision Air pia itaweka alama yake ya PW kwenye Ndege za Etihad zinazotoa huduma zake za kila siku kati ya Dar es Salaam na Abu Dhabi ikiwa ni hatua ya kuhimarisha uhusiano kati ya Afrika Mashariki na Falme za Kiarabu.

Kwa mujibu wa Ofisa Mkuu wa Mipango na Mikakati wa Shirika la ndege la Etihad, Kevin Knight, ‘Precision Air’ ni shirika lenye ubunifu wa hali ya juu ambalo limeweza kuibuka na tuzo mbalimbali katika utoaji wa huduma bora za anga.
Makubaliano yetu leo yanadhihirisha kuwa ndoto ya Shirika la Ndege la Etihad ya kuhimarisha huduma katika Ukanda wa Afrika Mashariki inazidi kukua.
“Huu ni mfano mzuri zaidi katika kuifikia mipango mikakati yetu ya kufanya kazi na wadau ili kutimiza dhamira yetu na kutoa huduma bora za kibiashara na usafiri wenye raha kwa chaguo bora zaidi,” aliongeza Ofisa huyo.
Naye Sauda Rajabu ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mkuu wa Precision Air Services PLC,alisema, “Hii ni hatua muhimu na mpya kwa Precision Air, na tunafurahi sana kufanya kazi na Shirika la Ndege la Etihad katika ushiriiano huu. Tunatazamia kuwakaribisha abiria wengi zaidi wa Shirika la ndege la Etihad kwenye ndege zetu na ni furaha yetu kuendelea kuzifikia fursa nyingi zaidi katika hatua ambayo itasaidia kuhimarisha uhusiano wetu kwa mipango ya muda mrefu.

“Kwa kupitia ushirikiano huu, tunawasaidia wateja wetu wa safari za ndani kujipatia fursa zaidi ya kwenda Abudhabi, na kusafiri maeneo zaidi ya 100 duniani kupitia mtandao mpana wa Shirika la ndege la Etihad ambao ni Afrika Mashariki ya Kati, Afrika, Ulaya, Asia, Australia na Marekani,”
Tangu jana abiria wameanza kukata tiketi za safari kutoka kwa mawakala au katika ofisi za mashirika haya kwa ajili ya safari za Januari 11, mwakani na kuendelea.

Shirika la Ndege la Etihad kwa sasa linatoa huduma katika nchi kumi barani Afrika 10 Afrika ikiwemo Johannesburg, Nairobi, Entebbe, Dar es Salaam, Khartoum, Casablanca, Rabat, Lagos, Cairo na Mahé, Seychelles.


 Kuhusu Shirika la Ndege la Etihad

Shirika la Usafiri wa Anga la Etihad (EAG) linafanya shughuli zake ulimwenguni kote likifanya biashara kupitia mashirika yake manne ambayo ni; Shirika la Ndege la Etihad, The National Airline of The United Arab Emirates, Etihad Engineering, Hala Group na Airline Equity Partners.
Shirika limewekeza kwenye mashirika saba mengine ambayo; Airberlin, Air Serbia, Air Seychelles, Alitalia, Jet Airways, Virgin Australia na Swiss-based Darwin Airline, inayofanya kazi chini ya  Etihad. 

Shirika la Etihad lenye makao makuu yake Abu Dhab limejiwekea malengo ya kuhudumia abiria  na usafirishaji mizigo maeneo zaidi ya  110 na kutoa huduma bora ya usafirishaji mizigo Mashariki ya Kati, Afrika, Ulaya, Asia, Australia na Amerika. Shirika lina ndege za Airbus na Boing 120, ikiwa na zingine 204 ambazo bado zinatumika kwa sasa;  ikiwamo  71 Boeing 787s, 25 Boeing 777Xs, 62 Airbus A350s na 10 Airbus A380s.

Kwa maelezo zaidi tembelea: www.etihad.com

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.