ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 25, 2016

AIRTEL YAWAPA SEMINA MAWAKALA MKOA WA MWANZA JUU YA HUDUMA MPYA YA AIRTEL MONEY TIMIZA.

Msimamizi mkuu wa uelimishaji wa huduma ya Airtel Money Timiza, Rwebu Mutahaba akitoa semina kwa Mawakala wa mihamala ya fedha za mtandao jijini Mwanza juu ya mikopo hiyo ya mtando wa Airtel ambayo imekuja kama sehemu ya maboresho ya huduma na kuwarahisishia wananchi wa Tanzania linapokuja suala la mtaji. 
Mawakala wa mihamala ya fedha za mtandao jijini Mwanza kwa umakini wakisikiliza mafunzo juu ya mikopo hiyo ya mtando wa Airtel ambayo imekuja kama sehemu ya maboresho ya huduma na kuwarahisishia wananchi wa Tanzania linapokuja suala la mtaji. 
Msimamizi mkuu wa uelimishaji wa huduma ya Airtel Money Timiza, Rwebu Mutahaba akitia msisitizo zaidi katika semina kwa Mawakala wa mihamala ya fedha za mtandao jijini Mwanza juu ya mikopo hiyo ya mtando wa Airtel ambayo imekuja kama sehemu ya maboresho ya huduma na kuwarahisishia wananchi wa Tanzania linapokuja suala la mtaji. 
Mawakala toka viunga mbalimbali ndani ya jiji la Mwanza wamekusanyika hapa ndani ya ukumbi wa Gold Crest Hotel kwa nia ya kupata mafunzo.
Somo limekolea na Airtel Money Timiza.
Airtel Money Timiza ni mikopo nafuu isiyo na masharti magumu zaidi ya namba ya mteja ya mawasiliano na historia ya utumiaji wa huduma ya Airtel Money Timiza.
"Ili mteja apate kukopeshwa kiwango kikubwa cha fedha, Airtel Money Timiza itatizama Je ni mteja anatumia vipi mahamisho na uchukuaji wa fedha kupitia Airtel Money yake...?
Kadri mteja anavyotumia Airtel Money zaidi ndivyo anavyopata nafasi ya kukopeshwa zaidi nacho kiwango kikipanda...." Somo la semina likiendelea
Washiriki kwa umakini na semina ya Airtel Money Timiza.
'MUDA NI MALI' = Jinsi Airtel Money Timiza inavyokomboa muda huku ikimkuza na kumnyanyua mwananchi toka lindi la umasikini.
Msimamizi mkuu wa uelimishaji wa huduma ya Airtel Timiza, Rwebu Mutahaba akitoa semina kwa Mawakala wa mihamala ya fedha za mtandao jijini Mwanza juu ya mikopo hiyo ya mtando wa Airtel ambayo imekuja kama sehemu ya maboresho ya huduma na kuwarahisishia wananchi wa Tanzania linapokuja suala la mtaji. 
David Wankuru ambaye ni Meneja wa Airtel Mkoa wa Mwanza akifafanua kilichofanyika ndani ya semina kwa mawakala, masharti na masuala yote juu ya Airtel Money Timiza.
 BOFYA PLAY KUMSIKILIZA.

Ni sifa zipi zitampa mteja fursa ya kuweza kukopeshwa na Airtel Money Timiza? Joel Laizer ambaye ni Meneja wa Mauzo Airtel Mwanza anafunguka zaidi.
 BOFYA PLAY KUSIKILIZA.
Mawakala - Kalunde Kafiti na wenzake hapa wanafunguka mengi juu ya
1.Wazo la Airtel Timiza linamanufaa gani kwa wenye kufanya kazi ya miamala?
2. Nini Tahadhari kwa matapeli wanaoweza kuitumia Airtel Money Timiza kufanya yao?
3.Jeh Mikopo itawasaidiaje wajasiliamali ambao suala la mtaji limekuwa changamoto kubwa kwao?
BOFYA PLAY KUSIKILIZA WALICHOSEMA.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.