ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 9, 2015

SABABISHA MAPINDUZI YA UCHUMI NA POSO KUPITIA MWONGOZO NA KUWA MTAYARISHAJI KWANZA

King Majuto aka Mzee Majuto akiwa ni mmoja wa wajumbe wa POSO (Point of Servise Office) Ofisi ya Huduma za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, akiwasilisha uzoefu wake wa kupambana na changamoto za ajira na kukuza kipato kwa baadhi ya wanahabari waliohudhuria Semina ya Siku moja iliyofanyika katika ukumbi wa G&G jijini Mwanza.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Bega kwa Bega Microfinance Co. Ltd BKB Bw. Albert P. Girenga akitoa taarifa kuhusu kampeni ya Sababisha Mapinduzi ya Uchumi na POSO kupitia Mwongozo wa kuwa Mtayarishaji kwanza.
Bwana Girenga amesema kuwa huduma wanayoitoa ni jitihada ya makusudi ya kuleta Mapinduzi makubwa ya Uchumi nchini Tanzania, ikiwa na dhana yenye fikra za kina na taswira pana ya mustakabali wa Watanzania kwa lengo la kumkomboa kiadilifu kila raia na vizazi vyake kutoka katika umasikini.

"Mafanikio ya mapinduzi haya yanategemea mshikamano wa walengwa, tunatumaini yatachangia kwa ujumla wamapinduzi haya na kuwafungulia jia ya kushiriki, wale watakaohamasika"

"Sababisha Mapinduzi ya Uchumi na POSO" ni kampeni ya kitaifa ya kufikisha kwa wananchi fursa za uwekezaji na uwezeshaji silisowekwa na sera hii kwa wananchi ili wazitumie kujitajirisha kiadilifu.

Kampeni hii inakusudia kujenga uelewa wa Watanzania walio wengi ili kushiriki kikamilifu katika ujenzi, umiliki, usimamizi na uendelezaji wa mitaji, vitegauchumi, soko, biashara na ajira.

Kupitia Kampeni hii kila Mtanzania atawezeshwa kuwa Mtajirishaji anayefanikisha ujenzi wa Nguvukazi Bora inayowajibika kutoa huduma, kuzalisha na kusambaza bidhaa bora zinazohimili ushindani katika soko la ndani na nje ya nchi.
Kwa kifupi, Mtajirishaji ni mtu mwadilifu, mwenye werevu wa kiwangocha juu cha kutumia mazingira yanayomzunguka na ya utandawazi kufungamana  katika ubia unaofanikisha uwekezaji unaoibua na kuendeleza Ubunifu, uvumbuzi na Ujuzi (UUU)unaobadili Wazo, taaluma na Rasilimali kuwa Huduma, Bidhaa na Mali Bora zinazouzika kwa Faida inayotengeneza Hazina ya kutajirisha vizazi vyote.
Kampeni hii ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa ujenzi wa ajira zinazowezesha wananchikufungamana na kujitajirisha kiadilifu, chini ya MILIKI mfumo wa UTAJIRISHAJI, unaoinua uwezo wa Watanzania, wa kubuni, kuanzisha, kuendeleza na kusimamia vitegauchumi nabiashara, kujenga na kumiliki mitaji ya uwekezaji, pamoja na kuhimili ushindani wa soko kwa kutumia rasilimali chache kati ya nyingi zinazotuzunguka.
Wabia wakuu katika utekelezaji wa mpango huu nikampunizilizoanzishwa na wananchi chini ya ushirikiano wa GODTEC (T) CO. LTD na Serikali kupitia Wizara ya Habari, Vijana, utamaduni na Michezo.
Meza ya wadau wa SUSO.
Wanahabari washiriki wa mkutano.








Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.