ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 26, 2014

KIMENUKA BUNGENI.

PAMOJA na maneno mengi yaliyosemwa, shutuma lukuki zilizotolewa na mbinu za kila aina kutaka kuzuia mjadala wa ripoti ya uchunguzi wa kashfa ya IPTL, hatimaye hii leo kila kitu toka kwenye uchunguzi wa kamati kimewekwa wazi jioni hii.


Taarifa ya kamati imeainisha nani mkweli na nani mwongo wakati Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), lilipowasilisha bungeni maoni yake kuhusu ripoti ya kuchotwa kwa Sh306 bilioni katika Akaunti ya Tegeta Escrow.
Uchunguzi huo ulifanywa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa maelekezo ya Serikali baada ya kuombwa na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila alipolalamikia ufisadi huo bungeni.
Pamoja na juhudi za kampuni ya IPTL na PAP kufungua kesi kuzua mjadala huo bungeni, hukumu iliyotolewa jana na majaji watatu ilisema kila kitu kiendelee kama kilivyo na kitakachoendelea kisiathiri kesi iliyopo mahakamani ambapo sasa mambo hadharani.
Moja kati ya MAPENDEKEZO MAKUU yaliyotolewa mara baada ya Taarifa hiyo kusomwa ni:- 
- Kufilisi mali zote za waliohusika ikiwa ni pamoja na hata wale waliohusishwa kwa nia njema.
-Baadhi ya walionufaika na fedha hizo ni viongozi wa Umma ambao wanapaswa kuzingatia sheria ya maadili ya viongozi wa Umma ikiwemo sheria namba 13 ya mwaka 1995 ambayo inawataka kutoa taarifa ya Zawadi wanazopata au Malipo wanayolipwa. Vyombo vya uchunguzi vitafanya kazi yake kuona kama Matakwa ya Sheria yalifuatwa....
 BOFYA PLAY KUSIKILIZA TAARIFA YA KAMATI 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.