ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 22, 2014

MEYA WA JIJI LA MWANZA MABULA AKABIDHI VIFAA TIMU 22 ZITAKAZISHIRIKI PEPSI KOMBE LA MEYA JIJI LA MWANZA 2014

Meya wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula (Wapili kulia) akionesha vifaa vitakavyo tumiwa na waamuzi wa mashindano ya Pepsi Kombe la Meya 2014 wa Jiji hilo, Meneja wa Kampuni ya SBC Nicolas Coertz (Kushoto) inayodhamini mashindano hayo.
Meya wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula (katikati) akipiga teke kibendera cha kona za uwanja kama sehemu ya kupima ubora wa vitendea kazi vya mashindano ya Pepsi Kombe la Meya 2014.
Meya wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula (Wapili kulia) akikabidhi seti kamili ya jezi kwa wawakilishi wa timu ya Mbugani inayoshiriki mashindano ya Pepsi Kombe la Meya 2014 wa Jiji hilo, Meneja wa Kampuni ya SBC Nicolas Coertz (Kushoto) inayodhamini mashindano hayo.
Meya wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula (Wapili kulia) akikabidhi seti kamili ya jezi kwa wawakilishi wa timu ya Nyamagana inayoshiriki mashindano ya Pepsi Kombe la Meya 2014 wa Jiji hilo, Meneja wa Kampuni ya SBC Nicolas Coertz (Kushoto) inayodhamini mashindano hayo.
Meya wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula (Wapili kulia) akikabidhi seti kamili ya jezi kwa wawakilishi wa timu ya Mkolani inayoshiriki mashindano ya Pepsi Kombe la Meya 2014 wa Jiji hilo, Meneja wa Kampuni ya SBC Nicolas Coertz (Kushoto) inayodhamini mashindano hayo.
Meya wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula (Wapili kulia) akikabidhi seti kamili ya jezi kwa wawakilishi wa timu ya Polisi inayoshiriki mashindano ya Pepsi Kombe la Meya 2014 wa Jiji hilo, Meneja wa Kampuni ya SBC Nicolas Coertz (Kushoto) inayodhamini mashindano hayo.
Daladala.
Igoma.
Pamba.
Mnadani.
Mstahiki meya wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula akizungumza na wanahabari.
Katika picha walioketi meza kuu wakifuatilia matukio uwanjani kutoka kulia ni Mstahiki meya wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula, Meneja wa Kampuni ya SBC Nicolas Coertz, Meneja wa Masoko wa Kampuni ya SBC Sharif Tak na Mkurugenzi wa Myway Entertainment Co. Paul Mganga (waandaaji wa mashindano hayo.)

TIMU 22, Waamuzi na Kamati ya Maandalizi jana wamekabidhiwa vifaa na vitendea kazi kwa ajili ya kuanza rasmi mashindano ya ya Pepsi Kombe la Meya wa Jiji la Mwanza 2014 jijini Mwanza.

Akikabidhi vifaa na vitendea kazi hivyo, Meya wa Jiji la Mwanza Stanislaus Mabula (CCM) ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mkolani alisema kwamba licha ya mashindano hayo kuwa na dhamira ya kukuza vipaji na kipato kwa wajasiliamali vijana kupitia zawadi kwa washindi, pia mashindano hayo yamelenga kujenga udugu,urafiki na mshikamano miongoni mwa wananchi wa jiji la Mwanza.

“Tutumie vizuri fursa hii hasa vijana kwa kucheza na kuzingatia kanuni na sheria za mashindano ili kupata ushindi utakaowezesha timu kupata zawadi ili kuwezesha kuwa na mtaji wa kujiendeleza katika ujasiliamali na vifaa hivi vitatolewa tena kwa timu zitakazoingia robo fainali na fainali ikiwa ni uboreshaji kwa mwaka huu,”alisisitiza.
Sharif Taki.
Kwa upande wake Meneja wa Masoko wa Kampuni ya SBC Sharif Taki inayodhamini mashindano hayo kwa mwaka wa pili mfululizo kupitia kinywaji chake cha Pepsi alisema kwamba, mashindano ya mwaka huu wameboresha zaidi udhamini wao kwa kuongeza timu kutoka timu 19 hadi kufikia 22 ikiwemo zawadi kwa washindi, ubora wa vifaa na vitendea kazi, huku michuano hiyo ikichezeshwa na waamuzi wanafunzi wa Kituo cha Soka cha Alliance cha jiji Mwanza.

Timu zilizokabidhiwa vifaa ikiwa ni seti kamili ya jezi, mipira miwili pamoja na nauli ya kufika katika kituo wakati wa mechi Sh.20,000 ambayo hutolewa siku timu inacheza, timu za Kata ya Mbugani, Nyamagana, Mkolani, Buhongwa, Butimba, Igogo, Mkuyuni, Mirongo, Pamba, Igoma, Isamilo na Mahina zile za Vikundi na Taasisi ni Magazeti FC, Wanahabari FC, Pilisi Jamii FC, Bodaboda, Sokoni, Mnadani, Fundi Gereji, Mwanza City FC, Machinga FC na Daladala FC.

Mashindano hayo yanayosimamiwa na Kampuni ya Myway Entartainment, yanataraji kuzinduliwa rasmi Agosti 2 Mwaka huu katika uwanjwa wa Nyamagano ambapo timu za Kata za Mkolani na Isamilo (Mabingwa) zitafungua dimba kabla ya timu zingine kuchuana katika viwanja vya Mabatini Polisi, Igoma, Mkolani, Buhongwa na Nyegezo kona ambapo timu zinetengwa katika makundi manne ambapo makundi ya A na C yatakuwa na timu sita na B na D yatakuwa na timu tano kila moja.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.