ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 18, 2014

KATIKA PICHA AJALI YA NDEGE YA MALAYSIA ILIYOUWA WATU 295.

Ndege ya shirika la Malaysian ikiwa na abiria 295 imeanguka Mashariki mwa Ukraine ikiwa safarini kutoka Amsterdam hadi Kuala Lumpur kukiwa na madai kwamba ilidunguliwa.
Rais wa Ukraine alielezea tukio hilo kuwa ni tendo la kigaidi huku waasi wakikanusha kuidungua. Inaaminiwa waasi hao wanaotaka kujitenga walizidungua ndege mbili za jeshi la Ukraine katika eneo hilo hivi karibuni.
Mabaki ya ndege hiyo ya shirika la Malaysian iliyoanguka na kuuwa abiria 295 .
Miili ya watu imetapakaa kila upande katika kile kinachoaminika kuwa masalia ya ndege hiyo ya muundo wa jet karibu na kijiji cha Grabovo, kinachodhibitiwa na waasi wanaotaka kujitenga,.
Ndege hiyo nambari MH17 ilikua inakaribia kuingia anga ya Urusi mawasiliano yalipokatizwa.
Passport zimebaki kama kumbukumbu na vielelezo vya abiria waliofariki dunia kwenye ajali hiyo.
Miili ya wahanga wa ndege hiyo, mizigo pamoja na mabaki ya ndege hiyo imetawanyika eneo la ajali. 
Anga ya Ukraine haikufungwa rasmi lakini mashirika ya ndege ya Ujerumani, Lufthansa, Air France ya Ufaransa na Uturuki,yanaliepuka eneo la Ukraine Mashariki.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.