ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 17, 2014

MWONGOZAJI, MWIGIZAJI MAHIRI BONGO MOVIE ADAM KUAMBIANA AFARIKI DUNIA.

Enzi za uhai wake mwigizaji Adam Kuambiana.
INAKUWA  vigumu kuamini kutoa taarifa kuwa yule muongozaji filamu maarufu ambaye vilevile ni mwigizaji wa filamu katika soko la Bongo Movie, Adam Kuambiana kuwa amefariki dunia.

Adam Kuambiana amefariki dunia wakati akipelekwa katika hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge jijini Dar es Salaam kwa matibabu alfajiri ya kuamkia leo.

Inatajwa kuwa kabla ya kuzidiwa marehemu alianguka chooni akiwa location katika hoteli ya Silver Rado iliyopo Sinza kwa Remy jijini humo ambapo kabla ya mauti kumfika, Adam alikuwa akilalamika kuwa anasumbuliwa na tumbo.

Kwa hivi sasa mwili wa marehemu uko katika mochwari za hospitali hiyo, ukisubiri taratibu nyingine za mipango ya kifamilia hatimaye kupumzishwa katika nyumba yake ya milele.

Taarifa zaidi tutaendelea kukufikishia kadri zitakavyokuwa zikitufikia.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI. AMEN!

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.