ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 7, 2014

WAKUU WA MAMLAKA ZA BIMA AFRIKA MASHARIKI WAKUBALIANA KUWA NA BIMA MOJA.

Mwenyekiti wa EAST ARFICA INSUARANCE SUPERVISORS ASSOCCIATION (EAISA) na Kamishina wa Bima wa Uganda, Alhaj Ibrahim Lubega Kaddunabbi akiongoza kikao cha wakuu wa Mamlaka za Bima kutoka nchi tano za Afrika Mashariki kilichoketi katika ukumbi wa Ray's Bay jijini Mwanza, kujadili na kupitisha uamuzi wa kuanzishwa utolewaji wa pamoja wa Huduma za Bima kupitia Makampuni ya Bima kutoka nchi tano wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki.
Kamishina wa mamlaka ya Bima nchini Tanzania Israel Kamuzora akishiriki kutoa mchango wake kwenye kikao cha wakuu wa Mamlaka za Bima kutoka nchi tano za Afrika Mashariki kilichoketi katika ukumbi wa Ray's Bay jijini Mwanza, kujadili na kupitisha uamuzi wa kuanzishwa utolewaji wa pamoja wa Huduma za Bima kupitia Makampuni ya Bima kutoka nchi tano wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki. Wengine katika picha kutoka kushoto ni Mr. Jonathan Gatera ambaye ni mwakilishi wa Gavana wa Benki ya Rwanda, Mrs. Agnes Ndirangu ambaye ni mwakilishi wa kamishina wa Bima wa Kenya, Mwenyekiti wa EAISA na Kamishina wa Bima wa Uganda, Alhaj Ibrahim Lubega Kaddunabbi na kulia ni mwakilishi kutoka Burundi Mr. Venant Kamana.
Mwenyekiti wa EAISA na Kamishina wa Bima wa Uganda, Alhaj Ibrahim Lubega Kaddunabbi akifafanua jambo mbele ya waancdishi wa habari (hawapo pichani).


Mwenyekiti wa EAISA na Kamishina wa Bima wa Uganda, Alhaj Ibrahim Lubega Kaddunabbi akifafanua jambo mbele ya waancdishi wa habari (hawapo pichani). Wengine pichani ni Mrs. Agnes Ndirangu ambaye ni mwakilishi wa kamishina wa Bima wa Kenya (kushoto) na Kamishina wa Mamlaka ya Bima nchini Tanzania Israel Kamuzora.
Akishiriki kuelezea uzoefu wa nchi yake katika utoaji wa Bima Mrs. Agnes Ndirangu ambaye ni mwakilishi wa kamishina wa Bima wa Kenya alisema taifa hilo lina kitengo maalum cha kukusanya na kusikiliza malalamiko na changamoto mbalimbali za Bima kutoka kwa wananchi ikiwemo Bima ya Afya ili kuboresha upatikanaji wa huduma bora. 
Waratibu wa kikao hicho kikazi zaidi.

WAKATI upatikanaji wa huduma ya Afya kupitia Mfuko wa Bima unaonekana kusuasua hapa nchini na wananchi wengi kusita kujiunga na mfuko huo kutokana na adha na usumbufu wanaoupata kwenye Idara a Afya pindi wanapohitaji kupatiwa matibabu wakiwa na Kadi za Bima ya Afya, hali ni tofauti kwa nchi za zingine zilizopo Jumuia ya Afrika Mashariki.

Hilo limebainika jana Jijini Mwanza katika Kikao cha Wakuu wa Mamlaka za Bima kutoka nchi tano za Jumuiya ya Afrika Mashariki kilichoketi kujadili na kupitisha uamuzi wa kuanzishwa utolewaji wa pamoja wa Huduma za Bima kupitia Makampuni ya Bima  kutoka nchi tano wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Akizungumza wakati wa kupitisha uamuzi huo Kamishina wa Mamlaka ya Bima nchini Tanzania Israel Kamuzora alisema kuwa bado zipo kasoro katika huduma inayotolewa kupitia Mfuko wa Bima ya Afya nchini kuonekana kusuasua kutokana na wataalamu wa Idara za Afya za serikali na binafsi kushindwa kutoa kipaumbele kwa wananchi walio na Kadi kupatiwa matibabu sawa na watu wengine wanaolipia gharama.

“Mfuko huu hapa nchini umeonekana kama vile watu waliojiunga kama vile ni msaada wakati katika mataifa mengine ya Ulaya, Amerika na Asia na baadhi Barani Afrika bila kuwa na Kadi ya Bima hupatiwi matibabu na Daktari au Mtaalamu lakini hapa kwetu wataalamu wanauliza kuwa analipia gharama ukijibu ndiyo unaanza kutibiwa na kudai una kadi unaelezwa subiri kwanza hili siyo sawa.”alisema.

Kamishna Kamuzora alisema kwamba bado serikali inatakiwa kutoa elimu kwa wataalamu na viongozi wa Hospitali, Vituo vya Afya na Zahanati kwamba wananchi wenye Kadi za Mfuko wa Bima ya Afya wapatiwe matibabu bila kujali kuwa na fedha tasilimu  huku pia ikidaiwa kuwa wanachama wengi wa mfuko huo hulalamikia usumbufu kwa kuelezwa na wataalamu wa Idara ya Afya baadhi ya vipimo havilipiwi na mfuko huo.

“Nchi zilizoendelea ukienda kwa Daktari na pesa anaweza kukukataa kukupatia matibabu kwa kuwa anatambua kuwa hutoweza kumlipa lakini ukiwa na Kadi atachangamka kukupatia huduma ya matibabu mara moja (First Class) kwa kutambua kuwa Kampuni ya Bima wanao uwezo wa kumlipa gharama za kutibu kutokujua kwetu isiwe ndiyo utaratibu, hivyo elimu iendelee kutolewa kwani sasa imeanza kueleweka” alisisitiza.

Kamzora aliongeza kuwa kwa sasa hapa nchini wananchi wameanza kuchangamkia zaidi wakiwemo walimu ambao awali waliweka mgomo na kukataa kukatwa mishahara yao ili kuchangia mfuko huo lakini hali ni tofauti kwa sasa wengi wao wanaisifia na kuwahamasisha wengine na wananchi kujiunga na mfuko huo lakini leo ukijaribu kuigusa kuwaondolea Bima ya Afya wengi wao watagoma kutokana na kuelewa faida zake.

“Japo itachukua muda kwani tumeelewa tuliko toka na hata kwenye Hospitali zetu wameanza kulitambua hilo lakini kikubwa zaidi ni kuhakikisha elimu inazidi kutolewa na kuwafikia walengwa ili kusaidia wengi kujiunga na mfuko huo wa Bima ya afya ili kupatiwa matibabu bila kunyanyaswa na itafikia wakati hata hao wa kulipia gharama kwa fedha tasilimu watapata usumbufu kutokana na Teknolojia”alisema Kamishna Kamzora.

Naye Jonathan Gatera ambaye ni Mwakirishi wa Gavana wa Benki Kuu ya Rwanda alisema kwamba kwa serikali ya  nchi ya Rwanda katika utoaji wa huduma ya Afya kwa wananchi wake inazingatia wale walio na Kadi za Bima ya Afya na serikali imekuwa ikihamasisha kwa kutoa elimu na asilimia kubwa wamejiunga na hutumia kupatiwa matibabu mpango ambao umekuwa na mafanikio makubwa.

Mjumbe kutoa Kenya, Agnes Ndirangu ambaye alimwakirisha Kamishna wa Bima wa nchini hiyo alisema kwamba Taifa hilo lina kitengo maalumu cha kukusanya na kusikiliza malalamiko na changamoto mbalimbali za Bima kutoka kwa wananchi ikiwemo Bima ya Afya ili kuboresha meanzisha upatikanaji wa huduma bora.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wakuu wa Mamlaka za Bima kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki Alhaj Ibrahim Lubega Kaddunabbi alisema kuwa kikao hicho kilichoketi kwa siku mbili kilikuwa kujadili na kupitisha maamuzi ya kuifanya Bima itumike kwa nchi zote wanachama wa Jumuiya hiyo badala ya kila nchi kuwa na utaratibu wake wa utohaji huduma za Bima na Viwango tofauti.

Alhaji Kaddunabbi ambaye ni Kamishna wa Bima wa nchini Uganda alisema kwamba lengo la kikao hicho ni kuhakikisha Makampuni ya Bima kushirikiana kwa pamoja kutoa huduma za Bima kwa pamoja badala ya kuwa na Bima ya kila nchi jambo ambalo limekuwa kero na adha kubwa kwa wananchi wanapoamua kutembelea nchi nyingine na kupata usumbufu wa kukata Bima upya ili kuruhusiwa kuingia nchi nyingine.

“Kwa sasa ukiwa na gari lako na BIMA ulilokata nchini Uganda ukienda nchini za Kenya, Tanzania, Rwanda na Burundi haitambuliki, tunalazimika kukata Bima tofauti, huu ni usumbufu ni vyema tukawa na utaratibu wa Makampuni na Mashirika ya Bima kutoa huduma hiyo na kukubalika na nchi zote wanachama, hata ukitokea umepata ajali basi upatiwe matibabu ukiwa nchi nyingine kwa Bima uliyokata nchi nyingine” alisema.

Katibu wa Wakuu wa Mamlaka za Bima (East Afrika Insurance Superviors Assocciation) kwa kifupi inafahamika EAISA, Venant Kamana kutoka nchini Burundi alisema kwamba Makampuni hayo ya utoaji wa Bima endapo yatafikia uamuzi wa kutoa huduma za pamoja kwa kushirikiana haitoathiriwa na uthamani wa fedha kwani Mabenki yaliyopo kila nchi yatatumika viwango vinavyojulikana kimataifa katika ubadilishaji wa fedha toka nchi moja hadi nchi nyingine za Jumuiya.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.