ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, February 26, 2014

USAID YAENDESHA ELIMU YA LISHE WILAYANI KONGWA MKOANI DODOMA

Katibu tawala wilaya Kongwa,Bw Joseph Kisyeli,akimywesha mtoto uji ulioongezwa virutubishi,katika kampeni za uhamasishaji wa chakula cha mtoto chenye virutubishi,katika kata ya ngomai. Zinazoendeshwa na  USAID Tuboreshe Chakula ambazo zilifanyika mjini humo.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Kongwa ,Bw Joseph Mwita Kisyeli,akihutubia wananchi juu ya umuhimu na faida za chakula kilichoongezwa virutubishi,kwa mtoto miezi 6 - miaka 5,katika kampeni ya lishe ilizofanyika kata Ngomai wilaya ya Kongwa chini ya udhamini wa na USAID Tuboreshe Chakula
Mkazi wa Kongwa  akimsikiliza kwa makini,Mtaalamu wa lishe toka USAID Tuboreshe chakula, Bi Mariam akielimisha faida na umuhimu wa virutubishi kwa mtoto umri wa miezi 6-miaka5.
Mtaalamu wa Lishe Bi Julita kutoka USAID Tuboreshe Chakula Project akimuelekeza mgeni rasmi katibu tawala wilaya Kongwa, Bw Joseph Kisyela umuhimu na jinsi ya kutumia Virutubishi ambavyo ni muhimu kwa watoto wenye umri wa miezi 6 hadi miaka 5. Sherehe hizo zilifanyika Wilaya Kongwa,kata ngomai mkoani Dodoma.
Baadhi ya kina mama wenyeji wa kijiji cha ngomai,wakishiriki zoezi la kunywesha watoto kampeni za lishe bora zinazoendeshwa na mradi wa USAID Tuboreshe chakula.
Kikundi maarufu cha ngoma wilaya kongwa kata ya ngomai,kikitumbuiza wakati wa sherehe za uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji wa virutubishi  zinazoendeshwa na USAID Tuboreshe Chakula katika kata ya Ngomai wilayani Kongwa.
Katibu tawala wa wilaya ya Kongwa na viongozi wenzake wakipata elimu zaidi kwa kusikikiza wataalamu wa lishe kutoka mradi wa USAID Tuboreshe Chakula katika kampeni za lishe zinazoendelea wilayani humo.
Timu ya wataalamu wa lishe kutoka mradi wa USAID Tuboreshe Chakula wanaoendesha kampeni ya lishe wilaya mbalimbali za hapa nchini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.