ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, February 26, 2014

MBUNGE AIRO AMTAKA DC WA RORYA KUACHA KASHFA PIA AWAACHE WATAALAMU WAFANYE KAZI YAO.

Na PETER FABIAN
MBUNGE wa Jimbo la Rorya Bw. Lamerck Airo amemvaa Mkuu wa Wilaya ya Rorya akimtaka kuacha kuwasha kuwashutumu wanasiasa kuwa ndo wanakwamisha ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ya Rorya na kuwakingia kifua wataalamu wanaofanya ubadhilifu wa fedha za umma.

Mbunge Airo alisema kuwa kitendo cha Mweka Hazina kufanya ubadhilifu wa milioni 111.7 na kuhamishwa huku baadhi ya Madiwani 16 wakibariki aondoke kwa kuhamishwa bila kuchukuliwa hatua jambo ambalo limeshangaza wengi wakiwemo Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo.

Airo pia ameitaka serikali kupitia Wizara ya TAMISEMI kuchua hatua za haraka kumrejesha Wilayani humo aliyekuwa Mweka Hazina wa Halmashauri hiyo Bw. Renatus  Mtasiwa baada ya kufanya ubadhilifu wa zaidi ya shilingi milioni 111.7 za Halmashauri hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Jijini Mwanza , Mbunge huyo alisema kwamba kutokana na kitendo cha kuhamishwa kwa aliyekuwa Mweka Hazina Mtasiwa kufanya ubadhilifu wa fedha za Ruzuku ya shule (Capitation) kiasi cha shilingi milioni 21, fedha za likizo za walimu kiasi cha shilingi milioni 90 kuzichota na kuzitumia tofauti na ilivyokusudiwa ni wizi ambao anatakiwa kuchukuliwa hatua kali za kimaadili na kisheria.

Bw. Airo alisikitishwa na taarifa za Mweka Hazina huyo, ambapo alidai kuwa siku mbili kabla ya Kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Rorya ambacho kiliketi hivi karibuni nayeye kushindwa kuhudhulia kutokana na kuwa kwenye majukumu mengine ya Kamati ya Bunge ambapo inadaiwa kuwapatia baadhi ya madiwani pombe na kuwalewesha kwa siku mbili ili kutomjadili na kuruhusu ahamishwe kama ilivyoelezwa kwenye kikao hicho.

“Nimesikitishwa sana na hili suala kwani Mweka Hazina alikuwa anakaimu Nafasi ya Mkurugenzi akitoka na muda mfupi akifanya ubadhilifu kwa kiwango cha fedha shilingi milioni 111.7 lakini alichokifanya akaenda kuomba uhamisho Wizarani na sasa kahamishiwa Hamashauri moja Mkoani Morogoro hivi hili kweli ni halali” alihoji kwa mshangao .

Aliongeza kuwa pamoja na kuwepo ubadhilifu huo baadhi ya Madiwani sita (6), Mwenyekiti wa Halmashauri ya Rorya Bw. Charles Ochele na Mkurugenzi halmashauri hiyo kwenye kikao hicho walitaka baraza liazimie kuchukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kumtaka arejeshe fedha za Likizo na Walimu alizotafuna lakini baadhi ya madiwani 16 kati ya 23 walidaiwa kuhongwa na kunyweshwa pombe kuwapinga.

Aidha Mbunge Airo alisisitiza kuwa suala hilo bado atalivalia njuga hadi kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri wa TAMISEMI Bi Hawa Ghasia ili kumshughulikia Mweka hazina huyo ikiwa ni pamoja na kumrejesha ili kurudisha fedha alizotafuna kama alivyo ahidi akijibu maswali ya baadhi ya wabunge waliotaka wezi kwenye halmashauri wasihamishwe na hata wakihamishwa warudi kujibu tuhuma zao za wizi.

Akizungumzia suala la Mkuu wa Wilaya Rorya kuwatuhumu moja kwa moja wanasiasa kuwa ndiyo wanakwamisha ukusanyaji wa makusanyo ya mapato ya Halmashauri ya Wilaya hiyo na kushuka kwa kiwango kikubwa, alisema kwamba hatua hiyo iliyojitokeza kwenye Kikao cha Kamati ya Ushauri Mkoa wa Mara (RCC) hivi karibuni ilikuwa na lengo la kupotosha ukweli kwa wajumbe wa kikao hicho.

Mbunge Airo alisema taarifa iliyozungumzwa na DC wa Rorya haikuwa na ukweli na inaonyesha anavyokurupuka kujibu hoja ambazo alipaswa kumachia Mkurugenzi kuzijibu ambaye ni Mtaalamu na mwenye kuwa na takwimu au hata Mwenyekiti na si yeye ambaye amekuwa mtu wa kudanganywa na kisha  kuzungumza vyombo vya habari bila utafiti wa kina.

“Nilimsikia akidai kuwa baadhi ya wanasiasa ndo wamechangia kushuka kwa ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri kupitia vyanzo vyake na alikwenda mbali kuwatuhumu wanasiasa bila hata kumshirikisha Mkurugenzi na Mwenyekiti Bw. Ochele kwani wao ndio walipaswa kujibu au ndiyo walikuwa na majibu sahihi ya kile kilichopelekea kushuka kwa ukusanyaji huo kwa mwaka wa 2013/2014 ya bajeti iliyopita.

Alifafanua kuwa kutokana na kauli hiyo, ameamua kuweka wazi kilichotokea kwenye Jimbo lake na Halmashauri hiyo kwa kueleza kuwa kwanza amesikitishwa na kauli aliyoitoa DC huyo ya kuwatuhumu baadhi ya wanasiasa lakini katika makisio ya bajeti ya mwaka 2013/2014 walipanga kukusanya shilingi milioni 615 za ada ya malipo ya kuuza viwanja, lakini hazikukusanywa na badala yake ilikusanywa shingi milioni 21,293,000/= tu.

“Hapa malengo hayakufikiwa sasa viwanja havikuuzwa kutokana na Serikali kushindwa kupeleka kwa wakati fedha ya kulipia fidia kama Halmashauri ilivyoomba  huku makusanyo ya ada baada ya kuuzwa viwanja ikiwa ya maombi ya viwanja hivyo ilikuwa ikusanywe kiasi cha shilingi milioni 12 na badala yake wamepata milioni 92.8”alisema

Aliongeza kuwa, makusanyo ya kodi za viwanja baada ya kuviuza walitegemea kukusanya milioni 16 zakini walikusanya shilingi milioni 5, 279,000/= tu sawa na asilimia 33 huku makusanyo ya ambayo ambayo hayakufikiwa ikiwa ni zaidi ya shilingi mia sita kutokana na kukosekana malipo ya fedha za fidia baada ya kucheleweshwa na serikali na kupelekea kushuka kwa makusanyo na mapato ya halmashauri hiyo.

Aidha ushuru wa maegesho ya Pikipiki kuna Kampuni ilipewa zabuni ya kuwa wakala wa kukusanya ambapo kwa mwezi inawasilisha shilingi 60,000/= jambo ambalo linashanghaza sana na ukizingatia kuna  kizuizi cha magari na pikipiki ambapo magari makubwa ya mizigo hulipia shilingi 30,000/=  na kufanya chanzo hicho nacho kushindwa kukusanya vyema mapato ya halmashauri hiyo.

“Hapa wanasiasa wanahusika vipi kuona mapato yanakusanywa na kampuni iliyopewa zabuni na kukusanya ushuru chini ya malengo yaliyokusudiwa halafu waheshimiwa madiwani wanapohoji wanaanza kusakamwa na mkuu wa wilaya kwamba ndo wanasababisha hili halikubaliki na tunasema mkuu wa wilaya hana weledi wa kuwashambulia wanasiasa na ache kufanya hivyo” alisisitiza.

Ametoa wito kwa wananchi kumuunga mkono katika kutetea haki za wana Rorya katika Halmashauri yao , Lakini pia amemtaka Mkuu wa Wilaya hiyo kuacha kuwasakama wanasiasa na kwamba wakati anateuliwa kwenda Wilaya ya Rorya alikuta tayari wao wamechaguliwa kuwatumikia wananchi na ikizingatiwa wao ni wana rorya hivyo aache tabia ya kukurupuka kuwasema hovyo na ache mara moja.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.