ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 13, 2013

VIONGOZI WA VYUO VIKUU NCHINI WAKUTANA JIJINI MWANZA NA KUJADILI MASUALA YA AJIRA.

Mhadhiri Mwanzamizi wa Uchumi ambaye pia ni Mtafiti na Mshauri mwelekezi toka Chuo Kikuu Mzumbe Dr. Honest Prosper Ngowi akitoa mada katika semina ya viongozi wa vyuo vikuu nchini waliokutana katika ukumbi wa jengo jipya la huduma ya maradhi ya Saratani  jijini Mwanza kujadili masuala ya fursa na upatikanaji ajira.
Ni sehemu ya wahudhuriaji wa semina ya viongozi kutoka vyuo vikuu vya mikoa mbalimbali hapa nchini waliokutana katika ukumbi wa jengo jipya la huduma ya maradhi ya Saratani  jijini Mwanza kujadili masuala ya fursa na upatikanaji ajira.
Ni sehemu ya wahudhuriaji wa semina ya viongozi kutoka vyuo vikuu vya mikoa mbalimbali hapa nchini waliokutana katika ukumbi wa jengo jipya la huduma ya maradhi ya Saratani  jijini Mwanza kujadili masuala ya fursa na upatikanaji ajira.
Kwa umakiiiini... yale yanayojiri.
Mhadhiri Mwanzamizi wa Uchumi ambaye pia ni Mtafiti na Mshauri mwelekezi toka Chuo Kikuu Mzumbe Dr. Honest Prosper Ngowi akitoa mada katika semina ya viongozi wa vyuo vikuu nchini waliokutana katika ukumbi wa jengo jipya la huduma ya maradhi ya Saratani  jijini Mwanza kujadili masuala ya fursa na upatikanaji ajira.
Kwa upande wake Rais wa TAHILISO Amon Chakushemeire, anasema kuwa changamoto kuu katika ajira kwa wahitimu nchini ni Takwimu, "Kama nchi hatujawa na 'DATA BASE' sehemu ambapo unaweza ukaenda ukaona kwamba mfano wahitimu wa shahada ya Sheria labda 6000, lakini soko la sheria la Tanzania linahitaji wanasheria 4000 ili hata wanafunzi wanaotoka kidato cha sita wanapokuja kuamua kusoma sheria wawe na taarifa kuwa wanakwenda kusomea kitu hali yake katika soko kiko hivi au vile"

Kisha akaongeza "Tulitegemea ukienda Wizarani taarifa hizo utazikuta kwamba wangapi wamechukuwa ajira nchini Tanzania lakini bado tunatatizo kubwa la Takwimu"
"Taasisi zinazo waandaa watu wanaopaswa kuingia kwenye soko la ajira na Taasisi zitakazo ajiri hawana mawasiliano mazuri, kila mmoja anatembe njia yake"

"Kwa hiyo Taasisi zinazo waandaa watu watakao ajiriwa haziwasiliani na yule atakaye waajiri ili aweze kuwaambia yeye angependa kupata mtu ambaye ana stadi zipi ili wanapokuwa wakiandaa mitaala waweze kuandaa mtu ambaye wanauhakika atakwenda kuuzika"
Katibu mtendaji wa TAHILISO Donati Sulla akizungumza na wanasemina kutoa miongozo.
Semina hii ni zaidi ya darasa.
Kwa nchi za Afrika tatizo la ajira hususani Tanzania hili lilipaswa kuwa liwe dogo nalisiwe kubwa kuliko nchi za Ulaya kwa sababu tuna rasilimali nyingi tuna mashamba (ardhi yenye rutuba), mito, migodi vyanzo vya nishati kama gesi na kadhalika kuliko hata nchi za Ulaya lakini limekuwepo kutokana na sababu za kihistoria kama ilivyokuwa miaka ya 1970 hadi miaka ya 80 ambapo mtu alikuwa akihitimu anasubiri kupangiwa sehemu ya kwenda kufanya kazi hivyo kukawa hakuna ubunifu wa kuvumbua vitega uchumi vingine vitakavyo toa ajira kwa umma wa sasa unaoongezeka siku baada ya siku.
Picha ya pamoja Mgeni rasmi Ally Msaki ambaye ni Mkurugenzi wa Ajira Wizara ya Kazi na Ajira (wa 5 kutoka kulia) ambaye alikuja kumwakilisha Waziri wa Kazi na Ajira, akiwa na Uongozi wa juu TAHILISO na wawezeshaji mada za ukosefu wa ajira.
Picha ya Pamoja.
The second.
Rais wa Serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu Cha KUHASS Bugando Mussa Mdede, ambaye pia ni rais mwenyeji wa mkutano huo akizungumza na vyombo vya habari. 
Mhitimu kutoka Chuo Cha Mtakatifu Agustino kitivo cha Elimu ambaye pia  ni Kamishna wa TAHILISO Kanda ya Ziwa Bi. Consolata Michael akizungumza na wanahabari. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.