ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, December 15, 2013

ELIMU YA TANZANIA VIJIJINI HALI TETE, UKATILI WAONGEZEKA KUTOKANA NA WENGI KUKOSA MAARIFA (ELIMU)


Vyumba vipatavyo SITA vya madarasa ya shule ya msingi Nyiboko iliyopo katika wilaya ya Serengeti mkoani Mara vimeezuliwa mabati kupitia mvua iliyoambatana na upepo kunyesha mnamo mwishoni mwa mwaka jana ambapo hadi leo wanafunzi wa shule hiyo wanasoma katika hali ngumu kwenye madarasa haya.

Jua linawatandika mchana kutwa wakiwa kwenye masomo, mvua ikinyesha wanafunzi wanatawanyika na wengine wakijisitiri kwenye kingo za baadhi ya madarasa yaliyosalia na mabati. Utoro kwa wanafunzi umekithiri hali iliyo sababisha wanafunzi wengine kuacha kabisa shule kukwepa kadhia hizo ikiwemo ya wanafunzi kukaa chini kwa kukosa kabisa madawati.

Akina dada wanao ikimbia shule hiyo wakikatisha masomo wanageukia biashara ya ukahaba wakiwa na changamoto ya kukosa elimu na kutojitambua na hata maamuzi yao ni ya kukurupuka ambayo mwisho wa siku yanasababisha ongezeko la ukatili wa kijinsia.   
Nilipofika shuleni hapa dakika chache mvua ilianza kunyesha, wanafunzi walikimbia toka madarasani na kuelekea kwenye madarasa machache yaliyo na kingizo za mabati na huyu aliamua kujisitiri hapa. Shule ya msingi Nyiboko ina takribani wanafunzi 1,200 lakini idadi ya wanaofika shuleni ni 200 na ushee.
Kwa mujibu wa mmoja wa wananchi waishio katika kata ya Nyiboko tarafa ya Ngulemi Bw. Mathayo Stephen akizungumza nami mara tu baada ya kumalizika kwa Mkutano wa semina ya utoaji elimu ya Ukatili wa Kijinsia inayoratibiwa na KIVULINI iliyofanyika katika viwanja vya shule hiyo amesema kuwa changamoto zilizo ikumba shule hiyo zimesababisha shule hiyo kongwe iliyojengwa miaka ya 50, kushuka kielimu.  Ukatili unaongezeka majumbani kutokana na watu kukosa elimu ...(Msikilize BOFYA Play)


Kabla ya kuezuliwa na upepo MEM ndiyo waliokarabati haya madarasa na mara, na kutokana na zoezi la ukarabati kuchelewa kufanyika tangu yalipoezuliwa na upepo kiasi cha mabati kilikunjwa na kuhifadhiwa store na kingine viongozi wakagawana, hivyo mpaka sasa idadi ya mabati yaliyosalia haitoshelezi madarasa.  
Shule ya msingi Nyiboko inachangamoto ya ukosefu wa walimu, ikiwa na mahitaji ya walimu 21 lakini walimu waliopo ni 9 tu.
Kwa mujibu wa mmoja wa wananchi niliye hojiana naye anasema kuwa diwani wa kata hii anayeitwa Donard Chacha Toghocho (CCM) inasemekana anakula kuku jijini Dar es salaam akiongoza kata yake kwa rimoti aka simu. Jeh! Ni nani atakaye inusuru shule hii kongwe iliyoanzishwa mnamo miaka ya 50 ambapo  leo hii vyumba vya madarasa vilivyo salia na mabati ni vitatu tu!?  Jeh! Wizara ya Elimu mmepata taarifa kuhusu hili? 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.