ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 13, 2013

ILI KUJENGEWA UWEZO WADAU WA MRADI WA UWAJIBIKAJI WA JAMII FORUM SYD WAKUTANA JIJINI MWANZA HII LEO.

Mkuu wa wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza Bi. Mary Tesha akizindua mpango wa Mpya wa Mradi wa Uwajibikaji wa Jamii wa Forum SYD mbele ya wadau mbalimbali wanaofanyakazi na mradi. Wengine katika picha kushoto ni Meneja Mradi wa Forum SYD nchini Tanzania Wawa, na kutoka kulia ni Mkurugenzi wa wilaya ya misungwi Bi. Naomi Nko pamoja na Mkuu wa wilaya ya Karagwe. 
Mkuu wa wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza Bi. Mary Tesha akimkabidhi kabrasha la mpango wa mpya wa Mradi wa Uwajibikaji wa Jamii wa Forum SYD, Meneja Mradi wa Forum SYD nchini Tanzania Wawa, mbele ya wadau wa mpango huo waliohudhulia semina ya kujengewa uwezo iliyofanyika katika Hoteli ya Victoria Prince jijini Mwanza. 
Wadau wa masualaya uwahia jambo toka kwa wawasilishaji mada. 
Washiriki wa semina hii ya ForumSYD ni kutoka maeneo ya mradi ambayo ni pamoja na wilaya ya Magu, Ukerewe na Karagwe.  
Akizindua mpango huo mkuu wa wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza Bi. Mary Tesha amewaagiza watendaji waliopo katika maeneo ambayo mradi huo unatekelezwa kushirikiana na wananchi ili walengwa waweze kunufaika na fedha zilizotengwa kwaajili yao katika kipindi cha 2013 hadi 2018.
"Uzuri wa Mfumo huu unapima uwezo wa jamii kutambua haki zao ili kutekeleza wajibu wao kwani kabla kufanyika kazi elimu hutolewa kisha unafuata utekelezaji" Mkuu wa wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza Bi. Mary Tesha akizungumzia mfumo ndani ya mpango mpya uliozinduliwa hii leo na Forum SYD jijini Mwanza.
Wadau wakisikiliza kwa makini kinachojiri kwenye semina hii.
Mkurugenzi wa wilaya ya misungwi Bi. Naomi Nko akizungumza na washiriki wa semina hii ya ForumSYD ambao wanatoka maeneo ya mradi ambayo ni pamoja na wilaya ya Magu, Ukerewe na Karagwe.
Wakifuatilia hatua kwa hatua ni sehemu ya washiriki wa semina hii ya ForumSYD kanda ya ziwa.
Wadau nao walipata fursa kuchangia kwa kubainisha changamoto au pengine ushauri juu ya nini kifanyike ili kuboresha.
Sauti ya mdau ikipaza kwa washiriki sanjari na meza kuu.
Kwa mijibu wa Meneja wa Mradi wa Forum SYD nchini Tanzania Godfrey Wawa unaofadhiliwa na serikali ya Sweeden mpango huo uliozinduliwa jijini Mwanza umelenga zaidi makundi yaliyosahaulika na jamii kama vila walemavu na waathirika wa virusi vya Ukimwi.
Shirika hilo limefikia uamuzi wa kuzindua mpango huo baada ya kuthibitika kuwa kumekuwepo na baadhi ya matukio kadhaa ya ukiukwaji wa haki za binadamu zinazo wanyima haki wananchi kushirikishwa katika maamuzi mbalimbali yanayo husu maisha yao, mazingira ambayo yanasababisha miongoni mwao kutopata kabisa haki za msingi.
Shirika la Forum SYD Tawi la Tanzania linalotekeleza wajibu wake chini ya mwamvuli wa serikali ya Sweden lilijitambulisha Afrika Mashariki miaka 30 iliyopita na kuanza utekelezaji wa miradi yake mnamo mwaka 1982.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.