ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 27, 2013

JANUARY MAKAMBA KUWA MGENI RASMI WA KONGAMANO LA KUJITAMBUA BODABODA MWANZA HII LEO.

Mwenyekiti wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoani Mwanza Makoye Kayanda akizungumza na waandishi wa habari (wanaonekana katika picha nyingine) amesema kuwa kutokana na kuwepo matukio mengi ya ajali, uporwaji wa Pikipiki, Wizi unaotokea kwa baadhi ya wateja unaofanywa na baadhi ya waendesha pikipiki wachache wasio waaminifu, uvunjwaji wa sheria unaotokana kutokuwepo elimu ya kutosha na Bima ya Afya wamelazimika kuandaa kongamano hilo.
Sehemu ya waandishi wa habari. 
Mwenyekiti wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoani Mwanza Makoye Kayanda akizungumza na waandishi wa habari.

MAKAMBA MGENI RASIMI WA KONGAMANO LA WAENDESHA PIKIPIKI (BODABODA) MWANZA.

KONGAMANO la Umoja wa waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza la kujitambua na kupata elimu ya huduma wanayoitoa kwa wananchi linatarajiwa kufanyika leo jijini Mwanza 

Kufuatia kutengwa kwa wanapopata ajali pia kukosa huduma za matibabu ni mambo yanayopelekea kuwepo semina hiyo maalumu kwa wanachama wao ikiwa ni pamoja na kuwahamasisha wengine kujiunga na umoja na mfuko wa Bima ya Afya Mkoani hapa.

Akizungumza na vyombo vya habari jana Mwenyekiti wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoani hapa Makoye Kayanda alisema kwamba kutokana na kuwepo matukio mengi ya ajali, uporwaji wa Pikipiki, Wizi unaotokea kwa baadhi ya wateja unaofanywa na baadhi ya waendesha pikipiki wachache wasio waaminifu, uvunjwaji wa sheria unaotokana kutokuwepo elimu ya kutosha na Bima ya Afya umesababisha uongozi wake kuandaa kongamano hilo.

Kayanda alieleza kuwa kufatia sababu hizo, Uongozi umeamua kuwashirikisha wanachama wake kujitambua na kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa taratibu, kanuni na sheria za Usalama barabarani hali inayopelekea kuwepo uvunjifu wa sheria kwa baadhi ya waendesha pikipiki hao na lawama kuwa za jumla hali ambayo imekuwa ikiwakosesha taswila na muonekano mzuri kwa jamii.

“Tumepata ajali nyingi sana za waendesha pikipiki kwenye maeneo mbalimbali na kupelekea kukosa huduma pale wanapochukuliwa baada ya ajali kupelekwa kupatiwa matibabu kwenye Hospitali na Vituo vya Afya ambapo wamekuwa wakipokelewa na kutelekezwa kutokana na watoa huduma kuwaona kama watu ambao hawafuati sheria na wasiokuwa na tawsila nzuri kwa jamii” alisema

Mwenyekiti huyo alisema kwamba uamuzi wao wa kuitisha kongamano hilo kwa kuitisha wanachama wao kutoka Wilaya zote za Mkoa huo ni kusaidia kutoa elimu kuwahamasisha kujiunga na mfuko wa Bima ya afya, kutii sheria bila shuruti na kukemea vitendo vya uharifu kwa wanachama na kuwabaini wanaofanya ili kuwafikisha kwenye vyombo vya dola na kuzingatia kanuni na sheria zilizopo.

“Tangu kuanzishwa rasimi kwa Umoja huo  na kupata usajili mwaka 2011 ukiwa sasa na wanachama wapatao 4461 Mkoani hapa na kupata mafanikio ya kupungua matukio ya upolwaji pikipiki ambapo kipindi kilichopita huko nyuma kabla ya umoja zaidi ya pikipiki 83 zilipolwa kwa waendeshaji na watu walioziuza mikoa mingine na kusababisha wimbi hili kushika kasi baadhi ya maeneo” alisema

Kayanda ametoa wito kwa jamii kuwapatia ushirikiano ikiwa ni pamoja na wateja wao kukubali kufuata sheria za kupanda pikipiki zao na kuvaa Kofia Ngumu za kujikinga na ajali pindi zinapotokea, kuwaunga mkono kuwatambua wasio wanachama na waendesha pikipiki waaminifu na wanaofanya vitendo vya uhalifu kuwatolea taarifa na siyo kuwaacha wakitumia kivuli cha waendesha pikipiki.

Aidha Kayanda, amewataka wananchi kuacha tabia ya kuishi kwa mazoea na kukubali kubadilika na kuzingatia pia sheria wakati wanapotumia huduma hiyo ambayo imekuwa na kusasambaa maeneo mbalimbali nchini kwa kisingizio cha kukataa kofio ngumu eti huambukiza majonjwa ya ngozi jambo ambalo halina uhakika na utafiti unaosemwa kutokana na taarifa zake kutokuwepo.

“Kongamano hilo la siku moja litafanyika katika uwanja wa nyamagana na kabla ya kuanza kutaongozwa na maandamano ya amani ya waendesha pikipiki kuanzia ofisi za Chama hicho zilizopo mtaa wa Mlango mmoja na yatapokelewa na mgeni rasimi ambaye ni Januari Makamba ambaye ni Naibu waziri wa Sayansi na Teknolojia (MB) kesho (leo) kisha kuwahutubia kabla ya kufungua kongamano hilo.


Ametoa wito kwa washiriki na wanachama kujitokeza kwa wingi huku pia waendesha pikipiki kuja kujiunga na umoja huo kwa lengo la kuboresha mambo mbalimbali ikiwepo kupitisha mkakati wa kupata mafunzo kutoka kwa vyombo husika na kuwasaidia kupata leseni na kuwa na utambuzi kwa wahusika.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.