ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 28, 2013

KWA MARA YA KWANZA KOMBE LA DUNIA KUIKANYAGA ARDHI YA JIJI LA MWANZA KESHO.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo, akizungumza na mbele ya waandishi wa habari na kamati ya maandalizi juu ya ujio wa Kombe la dunia ambapo jiji la Mwanza limetunikiwa nafasi ya kwanza nchini kulipokea kombe hilo. Wengine katika picha kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Dkt. Anthony Diallo na MNEC wa wilaya ya Tarime ambaye pia ni mkurugenzi wa Nyanza Bottling co. ltd, Christopher Gachuma. MSIKILIZE KWA KUBOFYA PLAY.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo, akizungumza na mbele ya waandishi wa habari na kamati ya maandalizi juu ya ujio wa Kombe la dunia ambapo jiji la Mwanza limetunikiwa nafasi ya kwanza nchini kulipokea kombe hilo. 
Mwakilishi wa Coca Cola Nchini bw. Eyebolt Gretchen (katikati) akizungumzia madhumuni  ya ziara iyo yenye lengo la kukuza mchezo wa soka.  Coca cola imemekuwa mstari wa mbele kwenye jitihada za kukuza soka nchini ikiwa imewekeza pia kwa vijana kupitia mashindano ya Kopa Coca cola.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Ernest Mangu amewahakikishia wanachi wote wa Mkoa wa Mwanza amani na utulivu, aidha amewaomba wananchi kutokuja uwanjani wakiwa na watoto wadogo ili kuepusha adha wanayoweza kupata watoto hao kutokana na msongamano.
Wadau wakiwa makini kusanyikoni.


Kwa mara ya kwanza Kombe la Dunia litapokelewa Mkoani Mwanza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uwanja wa CCM Kirumba.
  
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo, mbele ya waandishi wa habari na kamati ya maandalizi ya ujio huo katika ukumbi wa Mwanza Hotel hii leo.

Ndikilo amesema kuwa hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa kombe hilo kugusa ardhi ya mkoa wa Mwanza hivyo amewataka wanachi kujitokeza kwa wingi ili kuweza kunakshi na kutia mashamsham ya ujio wa kombe hilo lenye historia.

Naye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete ambaye yupo ziarani katika Mkoa wa Simiyu amekubali kuwa mgeni rasmi kulilaki kombe hilo litakalotua nchini katika ardhi ya mkoa wa Mwanza kisha jijini Dar es salaam.,

Amesema kombe hilo litawasili katika uwanja wa ndege wa mwanza majira ya saa tatu asubuhi na badae kupelekwa katika uwanja wa CCM Kirumba, ambapo pamoja na mambo mengine baadhi ya wananchi watapata fursa ya kupiga picha na kombe hilo.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Coca Cola Nchini bw. Eyebolt Gretchen, amesema ujio wa Kombe hilo kwa mara ya tatu katika nchi ya Tanzania umekuja kutokana na utulivu na amani iliyotawala nchini sanjari na ukarimu wa watu wake, Miongoni mwa nchi za Afrika ambazo zimekuwa na utulivu hata kufanya kutembelewa na kombe la Dunia ni Tanzania, amesema na kuongeza kwamba, kama Coca cola wamekuwa mstari wa mbele kwenye jitihada za kukuza soka nchini ikiwapo mashindano ya Kopa Coca cola.

Kwa upande wake kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Ernest Mangu amewahakikishia wanachi wote wa Mkoa wa Mwanza amani na utulivu, aidha amewaomba wananchi kutokuja uwanjani wakiwa na watoto wadogo ili kuepusha adha wanayoweza kupata watoto hao kutokana na msongamano.

Hii ni mara ya tatu kombe hilo kutua  nchini ambapo mara zote limekuwa likipokelewa na kulakiwa na wananchi waishio katika Mkoa wa Dar es Salaam. 

Ujio wa kombe hilo si tu kwamba linakuja kutazamwa na wananchi wa Mwanza bali pia ni fursa nzuri kwa mkoa huo kujitangaza kimataifa, kutangaza rasilimali zinazo patikana katika Mkoa huo na lakini pia ni chachu kwa vingozi kuona kuwa kuna umuhimu wa kuipa kipaumbele michezo yote. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.