ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, September 30, 2013

AIRTEL YAWANOA MAAFISA WA TRA JINSI YA KULIPIA ADA ZA LESENI ZA MAGARI KWA AIRTEL MONEY

Afisa huduma wa Airtel, Elly Mgumba akitoa mafunzo kwa wafanyakazi wa Tanzania Revenue Authority (TRA) juu ya matumizi ya Airtel Money kulipia ada za leseni za Magari. Mafunzo hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki hii katika ofisi za TRA zilizopo Mwenge jijini Dar es salaam na yataendelea tena wiki hii katika ofisi nyingine za TRA na mitaa mbalimbali dar es salaam

Afisa kodi wa TRA, Bw. Alex Dennis akijadiliana jambo na Afisa huduma wa Airtel Elly Mgumba muda mfupi baada ya kupewa mafunzo na mtaalamu huyo juu ya matumizi ya Airtel Money jinsi ya kulipia ada za leseni za Magari kwa Airtel Money

Airtel yawanoa maafisa waTRA jinsi ya kulipia ada za lesseni za magari kwa Airtel Money

•       Airtel yaendesha semina ya uelewa ofisi za TRA Mwenege -Dar es salaam
•       Mafunzo ya kulipia kodi kwa Airtel Money wiki hii kuendelea Manzese,
Tegeta Myfair kisha mikoa yote nchini

Mwishoni mwa wiki hii Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeendelea na ushirika wake na mamlaka ya mapato Tanzania TRA kwa kuanzisha semina za mafunzo kwaajili ya maofisa wa mamlaka hiyo ya jinsi ya
kurahisisha kukusanya mapato ya serikali kwa urahisi zaidi kupitia huduma ya Airtel Money

Mbinu pekee zinazoijadiliwa katika semina hiyo ni ile  yakuhakikishamlipa kodi yeyote anapata fulsa ya kufahamu njia rahisi na zenye kuokoa muda pale anapotaka kufanya malipo ya kodi mambali mbali ikiwemo  ya ada za lesseni za magari, ada za uamisho wa magari pamoja na malipo mengine ya ada za usajili wa magari

Mwishoni mwa wiki hii akiongea kuhusu ushirikiano huo wa Airtel Money na TRA kwenye ofisi za TRA MWENGE Afisa Mafunzo wa Airtel Bw, Elly Mgumba alisema “ tumeanza na wadau wetu wa TRA Mwenge-Dar es salaam lakini wiki ijayo tutasambaa mikoani ili wote wafahamu na waendelee
kuwaonyesha wananchi jinsi wanavyoweza kulipa ada zao

“Mteja akipiga *150*60# ataingia katika  orodha yetu ya Airtel Money na kwenda moja kwa moja kwenye neno TRAMAGARI na kufanya malipo papo hapo” alisistiza Bw, Mgumba

Kwa upande wake Meneja Mradi wa Airtel Money John Ndungu alisema “Mafunzo haya ya kulipia kodi kwa Airtel Money  wiki hii yataendelea katika  mitaa na ofisi za TRA Manzese, Tegeta Myfair na kisha kuingia kutoa elimu haraka kwa mikoa yote nchini  tukishirikiana na TRA idara  ya elimu kwa mlipa kodi”

Lengo letu Airtel ni kuwafikia walipakodi ambao wanatamani kuokoa muda kwa kuepuka kukaa foleni kwenye ofisi za malipo na sasa walipie kwa huduma hii ya Airtel Money rahisi na salama na kisha  kwenda kuchukua leseni zao kwenye ofisi yeyote ya TRA iliyopo karibu yako,  alimaliza kusema Bw Ndunguru

Nae Afisa kodi wa TRA, Bw. Alex Dennis Mwenge aliipongeza Airtel kwa jitihada zake za kuipunguzia serikali usumbufu wa kukusanya kodi na kuwawezesha wananchi kulipa kodi kwa hiari ili serikali iweze
kuendelea na mambo mengine ya maendeleo ya nchi

“Ninawapongeza sana timu ya Airtel Money kwa kuja kututembelea na kujadili jinsi tunavyoweza kuokoa muda wa mteja wa Airtel kulipa kodi kwa urahisi kwa njia hii ya Airtel Money sasa kwa pamoja tutahakikisha wananchi wanaokuja kulipa kodi kwa hiari wanafahamishwa kuhusu Airtel Money ili waweze kulipa kodi zao BURE wakiwa mahali popote nchini”

Airtel Tanzania kwa kushirikiana na mamlaka ya mapato Tanzania TRA ilizindua rasmi huduma ya kufanya malipo ya ada za  leseni za magari kupitia huduma ya Airtel money wiki mbili zilizopita. Huduma hii
inapatikana BURE yaani (Hakatwi Mtu Hapa) kwa wateja wote wa Airtel  nchi nzima.

Huduma ya Airtel money pia inawawezesha wateja kutumia simu zao za mkononi kulipa bill ya maji DAWASCO, kulipia Luku TANESCO malipo ya DSTV, kulipia visa ya USA na sasa ada za lesseni ya magari. Airtel money ni huduma rahisi na salama inayopatikana kwa kupiga *150*60#  na ufanye malipo mbalimbali.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.