ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 7, 2013

SAFARI BIKE RACE2013 KUFANYIKA KESHO SHINYANGA

SAFARI BIKE RACE 2013 KUFANYIKA KESHO MKOANI SHINYANGA

Mashindano ya mbio za Baiskeli kwa Kanda ya Ziwa yajulikanayo kama “Safari Lager Bike Race 2013” yanatarajiwa kufanyika kesho hapa Mkoani Shinyanga.

Shindano hilo ambalo limekuwa likifanyika kila mwaka kwa kushilikisha mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Mwanza, Tabora, Kigoma, Musoma, Kagera, Simiyu, Geita na Shinyanga limekuwa na mvuto wa kipekee kwa wanywaji na washabiki wa bia ya Safari Lager kwani kushiriki kutoka katika mikoa yote kwa kushindanisha mkoa upi kinara ya Kanda ya Ziwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Shinyanga mahali ambako mashindano yanafanyika, Meneja mauzo wa TBL Shinyanga, Robert Kazinza amesema kuwa lengo hasa la Bia ya Safari Lagera kudhamini mashindano haya ni kufufua mitaji ya wajasiliamali kanda ya ziwa kwani michezo ni ajira na zawadi za mashindano hayo ni kubwa. 

Mbio zitakazohusishwa ni pamoja na  mbio za wanaume ambao watakimbia Km 210, mbio za kimama Km 130, Mbio za walemavu wanaume na mbio za walemavu wanawake.

Pamoja na hayo chachu kuu ya mashindano hayo inatajwa kuwa itakuwa ni zile mbio za kiubunifu toka kwa akinamama watakao timua mbio na ndoo kichwani..
CHEKSHIA VIDEO INAYOFUATA HAPA CHINI:-


MWISHO.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.