ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 16, 2013

MKUTANO WA CHADEMA WA KUJADILI YA RASIMU YA KATIBA JINSI ULIVYOKUWA JIJINI MWANZA

Helikopta iliyowabeba viongozi wa CHADEMA ikiwa angani tayari kushuka kwaajili ya kuwahutubia maelfu ya wananchi waliofurika kwenye viwanja vya Magomeni kirumba jijini Mwanza kwa ajili ya mkutano wa hadhara wa kukujadili Rasimu ya Maoni ya Katiba. 

Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje akimtambulisha kijana ambaye anatajwa kuingizwa matatani akishinikizwa kukisaliti chama hicho kuwataja viongozi waandamizi wa chama hicho kuhusika katika mauaji mbalimbali na unyanyasaji nchini.

Chadema wameamua kuzunguka nchi nzima kwa lengo la kutoa elimu ya Katiba kwa wananchi, ikiwa ni pamoja na kutoa ufafanuzi wa maana ya Katiba na kujibu hoja za wananchi.

Wakishuka kuelekea jukwaani..

Mbunge wa Ubungo John Mnyika, alisema kuwa maadili ya uongozi na utawala bora, vinatikiswa kama siyo kuyumbishwa. Aliwataka wananchi kuhakikisha misingi ya taifa inarekebika kupitia marekebisho ya katiba mpya.
Mnyika alisema kuwa katika kupitisha maoni ya katiba, wanataka haki, uwazi na usawa katika masuala ya madini na rasilimali za nchi ambazo kimsingi zinapaswa kutajwa kwenye katiba. Tunataka Katiba pia impunguzie rais madaraka, alisema.
Alisema gharama za maisha ya wananchi zinazidi kupanda kila kukicha kutokana na rais kuwa na mlimbikano wa madaraka, hivyo kufanya maamuzi bila kutambua kuwa wananchi walio na kima cha chini ndio wanaoumia.
Aidha alisema kuwa anashangazwa na serikali ya CCM inavyokataa mfumo wa serikali tatu kwa madai kuwa,serikali tatu ni gharama kubwa sana kuendesha huku wakisahau baraza kubwa la mawaziri lisilo na meno.

Ni mikono kuonyesha idadi ya watu ambao hawajapata fursa ya kushiriki kuchangia mapendekezo ya rasimu ya katiba.

Red Brigade mkutanoni.

Mnyika alisema kuwa katika kuzungumzia Katiba hakuna vyama vya siasa, polisi wala mtu wa kada nyingine yoyote. Katiba ni mali ya Watanzania wote, hivyo kila mmoja ana wajibu wa kutoa maoni yake juu ya mambo anayoamini kuwa yatalisaidia taifa kama yataingizwa kwenye katiba.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema, kukusanya maoni ya wananchi kwa ajili ya kupata Katiba Mpya siyo kazi rahisi, ni kazi inayohitaji nia ya dhati ya taifa zima, kwa kuwa katiba ni mali ya wananchi na rasilimali za taifa.

Red brigade wakimzuia jamaa ambaye alikuwa akitaka kumfikia Mbowe huku akiwa na mabango yake wakihofia kuwa katumwa na watu wasiojulikana.

"Nataka nifike jukwaani..!!" Ilisikika sauti ya jamaa huyo.

Ilibidi nguvu zaidi iongezwe kutokana na jamaa huyo kung'ang'ania kufika jukwaani ili atimize azma yake.

Mbowe aliwasihi walinzi hao kumwachia, naye hatua kwa hatua akaelekea jukwaani akiwa amebeba mabango yake, mfukono akiwa amebeba vitu vizito.

Bango la Kwanza linamaanisha: 'Ona Chadema karibu mweshimiwa mkombozi wa haki zetu Mwanza, No Matata.'

Bango la pili lasema 'Hatumtaki Matata, Shashi No Matata...'

Mmenusurika Bukoba...!! Ndiyo ujumbe uliochomoza...

Acha wapigwe tu!! Ndiyo ujumbe uliochomoza...

Chadema imekuwa ikifanya mikutano ya hadharani nchini kuzungumzia mchakato wa katiba. Wamekuwa wakitoa elimu na kuwaeleza wananchi umuhimu wa kazi hiyo kwa taifa ambapo leo itakuwa ni zamu ya wakazi wa Mkoa wa Geita na wilaya zake.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.