ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 28, 2013

PICHA ZA MKUTANO WA UTOAJI TUZO ZA UTUNZAJI MAZINGIRA ZIWA VICTORIA UONAO ENDELEA USIKU HUU JB BELMONT MWANZA

Waziri wa Maingira Ofisi ya Makamu wa Rais Mh. Terezya Luoga akihutubia wadau wa mazingira na wamiliki wa viwanda eneo la Ziwa Victoria katika hafla ya utoaji tuzo kwa viwanda vilivyoimarika katika utunzaji wa mazingira Ziwa Victoria, shughuli imefanyika JB Belmont Hotel Mwanza. 

Tangu Julai 2010, kituo cha uzalishaji Bora na Hifadhi ya Mazingira Tanzania (CPCT) kikishirikiana na vituo mwenza vya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika mashariki kimekuwa kikihamasisha utekelezaji wa mbinu na teknolojia zenye kuleta ufanisi katika matumizi ya rasilimali na kupunguza uchafuzi wa mazingira katika viwanda na shughuli za kibiashara ndani ya bonde la Ziwa Victoria chini ya mwavuli wa Mradi wa Usimamizi wa Mazingira ya Ziwa Victoria - Awamu ya pili (LVEMP-II).

LVEMP-II ni mradi unaotekelezwa na nchi tano zinazozunguka bonde la Ziwa Victoria, hususan Burundi, kenya, Rwanda, Uganda na Tanzania, tangu September 2009 hadi Juni 2014.
Eneo la kusanyiko la wadau wa mazingira na wamiliki wa viwanda eneo la Ziwa Victoria katika hafla ya utoaji tuzo kwa viwanda vilivyoimarika katika utunzaji wa mazingira Ziwa Victoria, shughuli imefanyika JB Belmont Hotel Mwanza. 

Madhumuni makuu ya mradi kijenzi (Project sub-component) wa uzalishaji bora na upunguzaji uchafuzi wa mazingira (cleaner production) chini ya LVEMP-II ni kupunguza msongo wa mazingira ndani na pembezoni mwa Ziwa kwa kuzuia na kudhibiti vyanzo vya uchafuzi kutoka viwandani na kwenye shughuli za kibiashara kwa kutumia mbinu n ateknolojia mbalimbali za uzalishaji bora.
Hadi sasa viwanda na shughuliza kibiashara zipatazo 63 ndani ya Bonde upande wa Tanzania zimepata mafunzo kuhusu ufanisi wa matumizi ya rasilimali na upunguzaji wa uchafuzi yaliyoendeshwa na kituo cha Uzalishaji Bora na Hifadhi ya Mazingira (CPCT) na 20 miongoni mwao zimefanya tathimini ya uzalishaji bora (Resource Efficient & Cleaner Production Assessments)  kwenye maeneo yao na kutambua fursa mbalimbali za kuboresha shughuli zao.
Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula akitambulishwa kusanyikoni.

Wadau kwenye hafla.
Kampuni kumi kutoka Bukoba, Musoma na Mwanza zimeshiriki kakita kinyang'anyiro cha tuzo za RECP, 2013. Kampuni zote zinazawadiwa usiku huu vyeti na washindi watazawadiwa vikombe na /au vyeti maalum watakavyo tunukiwa na Waziri wa Nchi, ofisi ya Makamu wa Rais (Mazinrira) Mhe. Dr. Terezya Luoga Hovisa (Mb),kulingana na kiwango cha utekelezaji wa fursa za uboreshaji zilizokuwa zimeainishwa ili kushughulikia changamoto za ufanisi wa matumizi ya nishati,maji, malighafi na kuzuia ama kupunguza taka kwenye vyanzo.
Kuna aina tano za tuzo ambazo ni:- (i) tuzo ya kupunguza taka ngumu (Solidi waste reduction),
(ii) Tuzo ya kupunguza maji taka (Waste water reduction)
(iii) Tuzo ya ufanisi wa matumizi ya maji (Water use management),
(iv) Tuzo ya ufanisi katika matumizi ya nishati (kupunguza hewa ukaa)
(v) Tuzo ya mshindi wa Jumla (Overall Cooperate Award).

Lengo kuula Tuzo hizi (RECP Awards) ni kujenga kichocheo na mfumo wa kuwatambua wanaofanya vyema katika shughuli za viwanda na biashara kwa kuzingatia ufanisi wa rasilimali na kupunguza uchafuzi wa mazingira kama namna ya kuongeza tija katika uzalishaji, kupunguza uzalishaji wa taka, kuboresha usalama na afya kazini na kuongeza ushindani.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.