ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 22, 2013

KWA NGUVU ZOTE MEYA WA JIJI LA MWANZA AHAIDI KUKABILIANA NA CHANGAMOTO ZA ELIMU NA AFYA KATA YA MKOLANI.

Ni vijana  wa darasa la saba shule ya msingi Nyasubi ambao leo wameanza mtihani wa moko wakiwa kwenye majadiliano, Shule hii ni moja kati ya shule za kata ya Mkolani ambazo Mstahiki meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula amefanya ziara ya ukaguzi kimaendeleo.


Mstahiki meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula akizungumza na uongozi wa kata ya Mkolani ambapo alikutana na kamati ya Maendeleo ya Katanihumo WDC na kuelezea malengo ya ziara yake katika kukagua miradi ya maendeleo.


Kamati ya Maendeleo ya Katani humo (WDC) ikimsikiliza Mstahiki Meya aliyekuwa akielezea malengo ya ziara yake katika kukagua miradi ya maendeleo ikihusisha Sekta za Afya, Ekimu, Mazingira, miundombinu ya barabara, Maji na Umeme. 


Hapa Mstahiki meya wa Jiji la Mwanza Stanslaus Mabula akikagua Zahanati ya mtaa wa Mkolani.


Jengo la zahanati na huduma zikiendelea.


Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula akisaini kitabu cha shule ya msingi Ibanda, moja ya kero kubwa shuleni hapa ni ukosefu wa vyumba vya madarasa, ofisi za waalimu na madawati.


Nyuma ya darasa ya moja kati ya madarasa shule ya msingi Mkolani ni mbao za madawati yaliyovunjika kwa kukosa matengenezo huku watoto wakibanana kwenye mabenchi wakitegemea mapaja kama meza.


Hali jinsi ilivyo...


Hatuna madawati...


Idadi ya madawati na wanafunzi haviuwiani.

Mstahiki Meya na wajumbe wa kamati ya maendeleo ya Kata na baadhi ya wajumbe wa kamati ya shule wakimsikiliza mwalimu wa shule ya msingi Mkolani akielezea changamoto zinazoikabili shule yake.


Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula ameahidi kupambana kwa hali zote kuhakikisha mabadiliko yanafanyika ili kuboresha huduma zinazotolewa kata ya Mkolani.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.