ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, October 29, 2012

WAGOMBEA WAANZA KUJINADI NAFASI MBALIMBALI MZFA

Baada ya Kamati inayosimamia uchaguzi mkuu wa mkoa wa Chama cha soka mkoa wa Mwanza (MZFA) kuwapa rasmi barua wagombea wa nafasi mbalimbali hii leo kujulishwa kuanza rasmi kwa kampeni za uchaguzi kwa Chama hicho unaotarajiwa kufanyika Novemba 18 Mwaka huu baadhi ya wagombea wamebisha hodi kwa vyombo vya habari kuzinadi sera zao ili kuwapa mwanya wajumbe wa mkutano mkuu kuchanganua zipi pumba upi mchele.

Mmoja kati ya wadau wa michezo la jiji la Mwanza ambaye amekuwa akichangia maendeleo ya soka mkoani humo John Kadutu pamoja na kwamba amejitokeza kuwa mgombe pekee wa nafasi ya kuwa Mjumbe atakaye wakilisha vilabu vya mpira wa miguu mkoa wa Mwanza amewataka wajumbe kutumia busara wakati wa kupiga kura na kumpa kura zote za ndiyo...
Naye katibu wa Chama cha soka wilaya ya ilemela Juma Msaka akliyejitosa kuwania nafasi ya Katibu wa Chama Cha Mpira Mkoa wa Mwanza, sera yake imekuja na  Kauli mbiu ya 'Kutanua na kuendeleza soka mkoa wa Mwanza'
Mgombea wa mwisho kwa siku ya leo aliyejitokeza kujinadi huku wengine bado wakitafakari jinsi ya kunadi sera zao ni Aliyekuwa mchezaji wa zamani wa timu za Toto Africans, Cop United na Pamba zote za Mwanza. 

Si mwingine bali ni Katibu wa Chama cha soka wilaya ya nyamagana Munga Lupindo ambaye anagombea nafasi ya Ujumbe kamati tendaji ya Chama cha mpira wa miguu mkoa wa Mwanza

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. John Kadutu namkubali sana kama atapitishwa kama mwakilishi wa vilabu.
    Huyu jamaa ni mpambanaji hakuna mfano na Mwanza tutakuwa tumepata mjumbe asiye weza kukubali kuona maslahi ya Mwanza yanachezewa na TFF

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.