ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 17, 2012

MWANZA PRESS CLUB YAKAMILISHA SAFU YA VIONGOZI WAKE



MATOKEO

Rais wa Chama cha waandishi wa habari Tanzania UTPC Keneth Simbaya akihutubia Mkutano wa uchaguzi mdogo MPC
 Chama cha waandishi wa habari jijini Mwanza hatimaye kime kamilisha safu ya viongozi wake mara baada ya kufanyika uchaguzi mdogo uliofanyika jumatano august 2012 katika ukumbi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza kujaza nafasi za uongozi wa chama zilizokuwawazi.


 Nafasi zilizohusika na uchaguzi ni ya makamu mwenyekiti na mhasibu ambapo kwa nafasi ya Uhasibu ilishauriwa wagombea wawe wanawake pekee kwa kuwa katiba ilikuwa ikihitaji mwanamke kutokana na kwamba tayari nafasi tatu za juu zilikuwa na wanaume.


 Fredrick Katulanda aliyekuwa katika nafasi ya Uhasibu aliamua kujiengua ili kuleta changamoto za utendaji naye Flora Magabe aliamua kujiengua kukitumikia cha waandishi wa habari Mwanza katika nafasi ya Umakamu Mwenyekiti kutokana na kuelekeza mahaba yake zaidi kwa Chama cha Mapinduzi ambako kuna nafasi nyeti anagombea ndani ya CCM, na moja kati ya vipengele vya katiba ya MPC vinamtaka kiongozi kutokuwa na nafsi yoyote ndani ya vyama vya siasa.


Mwanahabari Emmy Lema akijinadi kwa wajumbe na wanachama wa MPC ili wampatie dhamana katika nafasi ya Uweka hazina licha ya kuwa na sifa za kutosha lakini kura hazikutosha. 


 Kura zikihesabiwa.


 Hatimaye Denis Mpagaze (kulia) ndiye alitawazwa kuwa Mwenyekiti msaidizi wa MPC kwa kura 38 akimwacha mpinzani wake Emmy Mshana aliyepata kura 9, kura zilizopigwa ni kura 47, kura 1 iliharibika. Pichani Mpagaze akiwa na Makamu mwenyekiti aliye jiuzuru Flora Magabe.


 Makamu mwenyekiti aliyejiuzuru kutokana na kuwa na mahaba na Siasa, Bi. Flora Magabe akipeana mkono na Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mwanza (MPC) aliyechaguliwa katika uchaguzi uliopita Deus Bugahirwa mara baada ya uchaguzi kukamilika. 


Safu kamili.
Nayo nafasi ya Uhasibu imenyakuliwa na mama Adventina Kashalaba (wa  pili mbele kutoka kulia) aliyemshinda Emmy Lema ambaye pia aligombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.