
Mkutano wa kujadili ukuzaji wa Shughuli za Utalii hapa nchini umefanyika mkoani Mwanza katika ukumbi wa mikutano Gold Crest ukiwa na malengo ya kutambulisha rasilimali za kitalii zilizopo Kanda ya ziwa ikiwa ni pamoja na kujadili juu ya kutambulisha utalii uliopo Mwanza, kuutanua utalii na kuzijadili changamoto za utalii zinazopaswa kuboreshwa.


Jiji la Mwanza kwa sasa lina makampuni ya kuongoza watalii yapatayo 28 ambao hufanya shughuli za kuongoza watalii ambao huja kujionea Mbuga za utalii zilizopo katika visiwa vya Ziwa Victoria, Hali ya hewa isiyo joto wala isiyo baridi, Vivutio vya Utamaduni na Historia vilivyopo jijini Mwanza pia ukaribu wa kuelekea mbuga ya Serengeti iliyopo mkoani Mara.

Changamoto kuu zinazoukabiri mkoa wa Mwanza ni pamoja na kutokuwepo uwanja wa ndege wa kimataifa pamoja na Mkoa bado haujachagua utalii wa Mwanza uongozwe na kitu gani.


Ili kuufikia utalii mkoani Mwanza ni Nchi zilizo karibu tu ndizo hutumia usafiri wa njia ya barabara ambazo ni Rwanda, Burundi pamoja na wageni watokao uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyata Nairobi nchini Kenya.

Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.