ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 14, 2012

MKUU WA MKOA WA MWANZA AFUNGUA MKUTANO MKUU WA CHAMA CHA SOKA MKOA (MZFA)

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. E Ndikilo akifungua mkutano MZFA.
Imetajwa kuwa kukosekana kwa uaminifu, matumizi mabaya ya madaraka sambamba na migogoro isiyoisha ndani ya vilabu na vyama vya michezo mkoani Mwanza ndiyo chanzo kikuu cha kuporomoka kwa michezo hususani soka kwa jiji la Mwanza.

Hayo yamebainishwa leo na mkuu wa mkoa wa Mwanza Injinia Ernest Ndikilo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Chama cha soka mkoa wa Mwanza (MZFA) unao kaa kila mwaka kuweka mikakati ya maendeleo na kujadili mstakabali mzima wa maendeleo ya soka.
Ongezeko la idadi ya watu na huduma mbalimbali za kijamii ile hali idadi ya viwanja inabaki palepale huku vingine vikibadilishwa matumizi imekuwa ni changamoto kubwa kwa mkoa wa Mwanza na wilaya zake.

Pia Mh Ndikilo hakuacha kuwapasha makocha wanaogeuza vyeti vyao mapambo ile hali walishiriki mafunzo ya Ukocha na fedha nyingi kutumika

Ili kurejesha heshima ya historia ya soka Mkoa wa Mwanza umeweka mikakati ya kuhakikisha unaingiza timu zaidi ya mbili katika ligi kuu zoezi ambalo litakwenda sambamba na uendelezaji wa vipaji vinavyochipukia.

Stori za ziada baina ya wajumbe wa MZFA na mkuu wa mkoa.

Picha ya pamoja.

Jumla ya wajumbe 33 kati ya 36 toka wilaya mbalimbali za jiji la Mwanza wamehudhuria mkutano huo wa mwaka uliofanyika katika ukumbi wa mikutano ukliopo ndani ya uwanja wa michezo CCM Kirumba Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.