ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 9, 2012

WAUGUZI 25,000 WALIOGOMA WAFUTWA KAZI KENYA

WAKATI wauguzi nchini Tanzania wakiwa kwenye mgomo usio na kikomo serikali ya Kenya imewafukuza kazi wauguzi 25000 waliogoma kwa kushindwa kurudi kazini.

Msemaji wa serikali Alfred Mutua ametoa wito kwa ‘ watu wenye taaluma ya afya wote’ ambao hawana ajira au waliostaafu kufika hosiptali za umma kwa ajili ya kuajiriwa siku ya Ijumaa.

Wafanyakazi wa umma ambo wengi ni manesi waligoma tangu wiki iliyopita wakitaka kupandishiwa mishahara, marupupurupu na kuboreshewa mazingira ya kazi. Kwa wastani mfanyakazi wa sekta ya afya anapata kiasi cha shilingi 25,000 zaKenya($300, £190) kwa mwezi kwenye mshahara wake na posho.

Bw Mutua alisema wafanyakazi wa afya ‘hawaufuata maadili’ kwa kutorejea kwenye majukumuyao. Majina ya wafanyakazi hao yameondolewa katika orodha ya wafanyakazi wanaolipwa mshahara na si ‘waajiriwa wa serikali tena’

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.