
Kile kipindi cha Daladala kinachorushwa kila siku kupitia ITV kikifanyika ndani ya Daladala ambamo humo abiria hujadiliana masuala mbalimbali yanayozunguka katika harakati za maisha yao ya kila siku, sasa ni zamu ya mkoa wa Mwanza hivyo basi ukikutana na Daladala maeneo ya Nyegezi, Kilimahewa, Pansiasi, Igombe, Igoma, Mabatini, Magu na kwingineko kote panda kisha husika....


Mdahalo umelenga kuainisha maeneo yanayohusiana na uhuru wa vyombo vya habari ni changamoto zipi, matatizo yapi, wapi kunahatarisha uhuru wa tasnia ya habari, ni namna gani ya kuikwepa hali hiyo na kila mtu anamajukumu yake iwe ni Mwandishi wa habari, wahariri wao, wamiliki wa vyombo vya habari, jamii kwa ujumla vyama vya siasa, serikali na nk kila mtu majukumu yake yameainishwa yote ni kwaajili ya kuboresha maisha yao kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.



Nashukuru sana vijana wenzangu kuonyesha uvumilivu wa hali ya juu katika mdahalo wa leo kwani katika mijadala mingi ya miaka ya sasa tumezoea kuona watu wakizomeana, kukatishana kabla mtu hajamaliza kuzungumza na mambo kama hayo...

ZE SAMPO YA KIPINDI KIDEONI MADA:-Ulevi na unyanyasaji wa kijinsia nchini Tanzania
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.