ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 10, 2012

DALADALAaaaaa MWANZA MPOoooooo!!

Daladala katika mitaa ya Mwanza.
Kile kipindi cha Daladala kinachorushwa kila siku kupitia ITV kikifanyika ndani ya Daladala ambamo humo abiria hujadiliana masuala mbalimbali yanayozunguka katika harakati za maisha yao ya kila siku, sasa ni zamu ya mkoa wa Mwanza hivyo basi ukikutana na Daladala maeneo ya Nyegezi, Kilimahewa, Pansiasi, Igombe, Igoma, Mabatini, Magu na kwingineko kote panda kisha husika....

Mtangazaji wa kipindi cha Daladala kinachorushwa kupitia ITV Daniel Kijo akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Mwanza Erenest Ndikilo, pindi crew ya kipindi hicho ilipodhuru ofisini kwa mkuu huyo jijini Mwanza leo tayari kuanza shughuli zake rasmi kuanzia wiki ijayo siku ya jumatatu.

Jenerali Ulimwengu akizungumzia mdahalo wa Uhuru wa vyombo vya habari uliofanyika leo katika chuo cha SAUTI Mwanza.
Mdahalo umelenga kuainisha maeneo yanayohusiana na uhuru wa vyombo vya habari ni changamoto zipi, matatizo yapi, wapi kunahatarisha uhuru wa tasnia ya habari, ni namna gani ya kuikwepa hali hiyo na kila mtu anamajukumu yake iwe ni Mwandishi wa habari, wahariri wao, wamiliki wa vyombo vya habari, jamii kwa ujumla vyama vya siasa, serikali na nk kila mtu majukumu yake yameainishwa yote ni kwaajili ya kuboresha maisha yao kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

Umma uliohudhuria mdahalo uliofanyika leo katika ukumbi wa mikutano Chuo Kikuu Cha Sauti jijini Mwanza.

Sahihi kwa kitabu cha mada kilichozinduliwa.

Mwanafunzi kutoka SAUT akizungumza na kipindi cha Daladala.
Nashukuru sana vijana wenzangu kuonyesha uvumilivu wa hali ya juu katika mdahalo wa leo kwani katika mijadala mingi ya miaka ya sasa tumezoea kuona watu wakizomeana, kukatishana kabla mtu hajamaliza kuzungumza na mambo kama hayo...

Kijana ukimpa nafasi na siyo kumwezesha tu, atasema kitu na hiyo nafasi itatumika na ninandoto kuwa siku moja uhuru wa vyombo vya utakuwepo kwani serikali itakuwa ikitenda kazi kwa wananchi na siyo serikari iliyo bosi kwa wananchi.

ZE SAMPO YA KIPINDI KIDEONI MADA:-Ulevi na unyanyasaji wa kijinsia nchini Tanzania

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.