ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, January 18, 2012

UZOEFU NA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI WAZEE KARAGWE NA MULEBA

MASHIRIKA yanayoshughulika na wazee wilayani KARAGWE (SAWAKA) NA KWA WAZEE MULEBA Yamefanya semina ya siku moja na waandishi habari mkoani Kagera kuona jinsi ya kushirikiana kufichua matatizo na kupata jinsi ya kukabiliana nayo kupitia vyombo vya Habari mkoani humo.

Akifungua semina hiyo Meneja wa mradi wa saidia wazee Karagwe Bwana Livingsote Bartholomeo Byekwaso, amesema lengo kuu ni kusaidia kufichua matatizo ya wazee pamoja na kutia chachu kwa serikali kutekeleza ahadi zake kwa wazee hao.

Naye Bi TEREZA EDWARD MINJA Mwenyekiti wa Tanzania Social Protection Netwaork akitoa tamko la wazee, katika semina hiyo amesema bado wazee wanalaumu serikali kutoweka sera ya wazee kisheria jambo linalosababisha matamko ya serikali kwa wazee hao kutotekelezwa kama matibabu bure na pensheni.

Mzee maarufu mkoani kagera na Tanzania ambaye ni mwenyekiti wa bodi ya kahawa Tanzania PIUS NGEZE amesisitiza kuwa serikali ijitahidi kuwajali wazee kwani wanapofika umri wa uzeeni afya zao zinakuwa na matatizo hivyo wasionekane bora wakiwa vijana uzeeni wakatengwa.

Wanahabari....

Hawa ni waandishi Habari mambo kwa upande wao wamesisitiza ushirikiano wa mashirika ya saidia wazee Karagwe na Muleba kutoa ushirikiano na wanapokuta tatatizo sehemu wawe tayari kuwajulisha waandishi ili wayatangaze lakini kubwa zaidi washirikiane kuwezeshana kufika maeneo korofi.
PICHA na Nicolaus Ngaiza
Radio Kasibante.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.