ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, January 18, 2012

ONYESHO MAALUM KUMUENZI MSANII ALIYEUAWA MWANZA KUFANYWA NA WASANII WA MWANZA JUMAPILI HII NDANI YA STONE CLUB

Kwanza kabisa naomba radhi wadau wote wa Blogu hii kwani nilishindwa kufikisha taarifa hizi mapema mtandaoni kutokana na kupigwa butwaa kwa msiba uliotokea, kwangu ilikuwa ngumu kuamini kuwa mdogo wetu katutoka... ingawa nilikuwa napata muda wakutundika taarifa nyingine mtandaoni lakini kwa hili moyo ulikuwa mzito.. mzito nikihisi ni kama mchezo wa kuigiza hivi... Kumbe kweli Mo-Chella hatunaye na leo imenibidi kuandika...Marehemu Mo-Chella katika safari yake ya mwisho.
KWA UFUPI.
Mwana bongo fleva wa hip hop toka Rock City Frank Buchella aka Mo-Chella alifariki dunia tarehe 12/jan/2012 kwa kuchomwa kisu cha chemba ya moyo katika eneo la mitaa ya Nera na jamaa mmoja dereva wa bodaboda aliyefahamika kwa jina la Christopher au Alliance Tota au Baba Keja. Ili kuingiza matirio wakati alipokuwa akijisomea kwa mitihani aliamua kwenda kuamua ugomvi wa jamaa huyo aliyekuwa akizozana na mwanamke mmoja na ndipo mauti yalipo mkuta

Mo-Chella ambaye pia aliyekuwa mwanafunzi wa CBE Mwanza amezaliwa tarehe 10/march/1989 na kuzikwa tarehe 14/jan/2012, mazishi yake yalishuhudiwa na watu wengi akiwemo Mkuu wa wilaya ya Ukerewe Queen Mlozi, Mbunge wa Ukerewe Salvatory Luyaga Machemli (CHADEMA), wasanii wenzake toka familia ya muziki wa bongo fleva Mwanza inayojulikana kwa jina la Mwanza Kwanza na wadau mbalimbali.


D-Malik(L) akiwa na marehemu Mo-Chella(R)
ONYESHO MAALUM LA KUMUENZI KUFANYIKA JUMAPILI HII
Kutokana na msiba huu wasanii wote wa Mwanza kutoka katika familia ya Mwanza Kwanza chini ya mwenyekiti wao Philbert Kabago watafanya Tamasha la kumuenzi marehemu Mo-Chella, litakalofanyika Jumapili 22/jan/2012 ndani ya ukumbi wa Stone Club kuanzia saa nane mchana hadi saa mbili usiku, kiingilio shilingi 2000/=

Mapato yote yatakayopatikana yatapelekwa kwa mama wa marehemu ikiwa ni kama njia ya kumfariji na kutambua mchango wake katika sanaa.

Alipokuwa akihojiwa studio za Passion Fm
Mo-Chella ambaye alikuwa akitegemewa kurithi mikoba ya wakali kadhaa wanaosikika na kutamba wakiwakilisha Rock City tayari alikwisha fanya ngoma zake kadhaa katika studio mbalimbali ikiwemo A2P, Mo-Records na Young Don Production atatakumbukwa kwa kuyatendea vyema majukwaa mbalimbali ya ushindani jijini, Mwanza show yake ya mwisho alipiga tarehe 31/dec/2011 usiku wa kuukaribisha mwaka mpya 2012 ndani ya Stone Club ambapo alipanda jukwaa moja na Suma Lee mara baada ya kupigiwa kura nyingi na mashabiki wa 91.0 Passion Fm wiki moja kabla ya show hiyo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.