
Warsha ya siku tatu ya kukusanya maoni ya wadau kuhusu hali ya maisha ya mtoto anayeishi mazingira ya mijini inayofanyika jijini Mwanza imebaini kuwa, Athari nyingi zinatajwa kuwa zitaendelea kuwakumba watoto wengi nchini kutokana na wazazi wengi kukosa nafasi ya kuwalea watoto katika makuzi bora sambamba na kuwaacha bila malezi.


Taarifa zinakusanywa hapa ili baadae zijumuishwe kwenye mpango mkakati wa UNISEF kusaidia watoto kutoka kwenye lindi la manyanyaso ili waishi maisha stahiki.

Mazingira ya nyumbani yanaweza kuwa si rafiki kwa mtoto yaani hayatoi fursa kwa mtoto kujisikia kuwa yuko huru kupata huduma nzuri toka kwa wazazi ikiwemo kusikilizwa.


Serikali imeweka mpango kwa kila kata kuwa na askari kwaajili ya kupata taarifa juu ya mipango yote ya uhalifu.

Wadau wajikite kwenye stadi za malezi ya watoto ili kuwanusuru watoto dhidi ya tabia chafu zitakazo isababisha nchi kupoteza uelekeo wa maisha ya baadaye.

Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.