ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 26, 2011

KUSHEREKEA MIAKA 50 YA UHURU PSI YAJUMUIKA NA WADAU WAKE UFUKWE WA ZIWA VICTORIA

Timu ya wafanyakazi wa PSI Musoma katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa michezo mbalimbali katika ufukwe wa Tunza, mara baada ya kusanyiko la shirika hilo lililofanyika jijini Mwanza.
Timu ya wafanyakazi wa PSI wilaya ya Bunda wakipata flash ya pamoja.
Mchezo wa kwanza ulikuwa ni soka Musoma v/s Bunda ambapo matokeo timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 2-2.
Mchezaji wa timu ya PSI Bunda (light green bips) akishindana kwa mabavu kuunasua mpira mbele ya beki wa timu ya Musoma (orange bips).
Hadi mwisho timu hizo zilitoka sare ya 2-2
Kona ya wafanyakazi mashabiki.
Katika mchezo wa voleball Musoma waliibuka kidedea.
Kuvuta kamba wanawake Timu ya Bunda iliwashinda mabavu Musoma.
Mkurugenzi wa (PSI) Population Services International Tanzania.
PSI imekuwa ikifanya kazi kuboresha afya ya Watanzania tangu mwaka 1993. Ni shirika linalo tumia mbinu mbalimbali kuhamasisha sekta binafsi kuwa na tabia ya kuupa mwili lishe kwaajili ya afya likitoa misaada ya chakula mashuleni, na kutoa elimu kwa wananchi hasa vijijini kufanya kazi kwa ajili ya masoko ya maskini.

Bunda walitia fora katika dancing competation ya Kwaito na kiduku ambapo ni moja kato ya michezo mitatu ya muziki iliyoshirikishwa mahadhi mengine yaliyohusishwa ni muziki wa Sebene.
Mambo ya twisti
Anicet ambaye alikuwa mratibu wa Tamasha hilo lililofanyika Tunza beach mkoani Mwanza, akishiriki timu ya PSI Bunda hapa alikuwa akimwaga shukurani zake kwa wadau wenzake kwa lugha ya Kihindi.

PSI ni shirika linalofanya kazi katika nchi zaidi ya 60, na makao yake makuu ni mjini Washington DC.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.