

Miongoni mwa changamoto hizo ni kuharibika kwa mara kwa mara kwa mashine za X-Ray uchakavu wa mashine ya CT Scan na upungufu wa nyenzo zinazo hitajika katika upasuaji wa moyo na ubongo.

Amesema Hospitali hiyo inatarajia kuchangisha fedha desemba pili mwaka huu kutoka kwa wadau wa sekta ya afya ili kukabiliana na changamoto hizo.
Kwa takribani miezi mitatu iliyopita hospitali hiyo imekumbwa na tatizo kubwa la uhaba wa gas aina ya oksijeni hali iliyosababisha kukwama kwa zoezi la ufanyaji operesheni hata kusababisha watu kadhaa wakiwemo watoto kupoteza uhai.
Sababu za hali hiyo zinatajwa kuwa ni deni iliyokuwa ikidaiwa hospitali hiyo na kiwanda cha kuzalisha gesi hiyo nchini.
Kwa sasa kupitia ufadhili wa wizara ya afya umesaidia kwa kiasi kurejesha hali ya kawaida ya huduma ya upasuaji hospitalini hapo ingawa kuna changamoto ya kiwanda cha kuzalisha gesi ya oksijeni kurejea katika uzalishaji kwa viwango visivyokidhi mahitaji.

Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.