ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, October 25, 2011

BREAKING NEWZ: WATU ZAIDI YA 20 WAHOFIWA KUFA MARA BAADA YA BASI KUTEKETEA KWA MOTO MKOANI PWANI

Watu kadhaa wamefariki dunia katika ajali mbaya ya basi la abiria iliyotokea kibaha mkoani pwani kamanda wa polisi wa mkoa huo ERNEST MANGU amesema kwamba idadi ya vifo kwa ajali hiyo iliyo husisha gari la Deluxe lililokuwa likitokea jijini Dar es salaam kuelekea mkoani Dodoma liliungua na kuteketea kabisa kwa moto.

Habari ambazo hazijathibitishwa inasema kuwa idadi ya waliokufa inaweza kuwa zaidi ya watu ishirini.

Imeelezwa kwamba idadi ya abiria walioondoka na basi hilo kutoka katika kituo kikuu cha mabasi ya mikoani Ubungo jijini Dar es salaam walikuwa arobaini na mbili lakini basi hilo linauwezo wakubeba abiria sitini na tano.

Hata hivyo msemaji wa hospitali ya Tumbi mkoani Kibaha Rose Mtei amesema kuwa mpaka jioni hii wamepokea majeruhi thelethini na tano wa ajali hiyo ambapo kumi na tatu wameruhusiwa, wengine wakiendelea kupatiwa matibabu zaidi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.