ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 25, 2011

"CHEREKO CHEREKO UMEPONA MAZEEEE!!"

Jana katika ofisi za Nishati na Matini kulikuwa na furaha ya hali ya juu baada ya Mhe. Jairo kuwasiri katika kibarua chake kilicho ponea chupu chupu kutiwa mchanga na wabunge

KATTIBU MKUU KIONGOZI, Phillemon Luhanjo(kulia) alitangaza uamuzi huo katika mkutano wake na waandishi uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam juzi akisema Jairo hana hatia na jana anapaswa kurejea kazini mara moja.

Alisema matokeo ya uchunguzi dhidi yake yamebainisha kwamba hakuwa na hatia hivyo kusema kwa mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa Sheria namba 8 ya Utumishi wa Umma ya mwaka 2002 na kanuni zake za mwaka 2003, anamrejesha kazini Jairo... “Ninaamuru David Jairo arejee kazini kuanzia siku ya Jumatano (jana).”

KUMBUKA kuwa..... tuhuma hizo zilitolewa na Mbunge wa Kilindi (CCM), Beatrice Shellukindo na hata kumfanya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuzitolea maelezo Bungeni akisema akama angekuwa na mamlaka, angelitolea uamuzi (kumwajibisha mhusika) lakini akaahidi kulifikisha kwa Rais ambaye alisema ndiye mwenye mamlaka ya uteuzi.

Tehe! mwisho wa siku shangwe kama kawaiiiida'


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.