Jamaa anaye tambulika kwa jina la Juma Hemed Hamisi (pichani)anatafutwa na Jeshi la polisi mara baada ya kutoweka na kiasi cha pesa shilingi za kenya 115,000/= (lakimoja kumi na tano elfu) sawa na shilingi za Tanzania 2,127,500/= (milioni mbili lakimoja na ishirini na saba elfu na miatano), pamoja na pesa taslimu za kitanzania shilingi laki tatu alizokabidhiwa kwaajili ya kufanya malipo mbalimbali.
Dreva Juma Hemed Hamisi inatajwa kuwa alipofika mpakani aliliitelekeza gari hilo lenye namba za usajili T106 ABQ roli aina ya Scania mali ya Lakairo Investiment likiwa na mizigo yake, akitokea nchini Kenya kuingia Tanzania.
Taarifa za tukio la kutoweka kusiko julikana kwa dreva huyo huku akiwa na mafungu ya watu yaani jumla ya fedha ikiwa ni shilingi milioni mbili laki nne ishirini na saba na mia tano, akimwacha mwajiri wake mdomo wazi asijuwe kisa na mkasa tayari zimeripotiwa kwa jeshi la polisi kupitia RB no MZN/RB/5347/11.
Roli lililotelekezwa tayari limekwisha fikishwa kwa mwenye mali mara baada ya dereva mwingine kuagizwa kulifuata mpakani. pichani likiwa kwenye karakana ya Lakairo Investiment, Mwaloni Kirumba jijini Mwanza
RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA
-
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe.
Mwanaidi Ali Khamis akigawa iftar kwa mmoja ya mtoto anayelelewa katka
Makao ...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.